Monday 27 October 2008

RONALDO ATWAA TUZO YA FifPro WORLD FOOTBALLER OF THE YEAR!!!




Cristiano Ronaldo wa Manchester United leo ameshinda Tuzo ya kuwa MCHEZAJI BORA WA DUNIA kwa mwaka huu iliyotolewa na FifPro ambacho ni Chama cha Wachezaji wa Kulipwa Duniani.
Ronaldo amewashinda kina Lionel Messi, Fernando Torres, Xavi na Mchezaji mwenzake wa Manchester United Rio Ferdinand katika kinyang'anyiro hiki ambacho Wachezaji wa Kulipwa kutoka zaidi ya Vyama 40 duniani vilimpigia kura.
Ronaldo ambae msimu uliokwisha alifunga jumla ya mabao 42 aliweza kuisaidia Timu yake Manchester United kutwaa Ubingwa wa LIGI KUU UINGEREZA na wa Ulaya mpaka sasa ameshatwaa Tuzo za Mchezaji na Mfungaji Bora LIGI KUU UINGEREZA pamoja na Mchezaji na Mfungaji Bora wa Klabu za Ulaya ya UEFA.
Ronaldo ametoa shukrani zake kwa FifPro kwa kutamka: 'Kutambuliwa na Wachezaji wenzangu wa kulipwa zaidi ya 50,000 duniani kote ni maajabu! Napenda nitoe shukrani zangu za dhati kwa Wachezaji wenzangu wa Manchester United, Makocha wangu wa Klabuni na Timu ya Taifa, familia yangu na marafiki zangu!'
Alimalizia kwa kusema: 'FifPro naipongeza kwa kazi nzuri ya kutetea na kuboresha maslahi ya Wachezaji wa kulipwa. Nawashkuru kwa Tuzo hii!'
Ronaldo vilevile yuko kwenye kinyang'anyiro cha kugombea Mpira wa Dhahabu [yaani Ballon d'Or] na Tuzo ya MCHEZAJI BORA DUNIANI YA FIFA 2008.
Vilevile FifPro imeitangaza Timu yake Bora ya Mwaka 2008:
KIPA– Iker Casillas (Spain/ Real Madrid) WALINZI– Sergio Ramos (Spain/ Real Madrid), John Terry (England/ Chelsea), Carles Puyol (Spain/ Barcelona) and Rio Ferdinand (England/ Manchester United) VIUNGO- Steven Gerrard (England/ Liverpool), Xavi (Spain/ Barcelona) and Ricardo Kaká (Brazil/AC Milan). WASHAMBULIAJI– Lionel Messi (Argentina/ Barcelona), Fernando Torres (Spain/ Liverpool), and Cristiano Ronaldo (Portugal/ Manchester United)

No comments:

Powered By Blogger