
Mwenyekiti wa Tottenham Hotspurs Daniel Levy [pichani kushoto akiwa na Ramos] ametoa utetezi wake kumfukuza kazi Meneja Juande Ramos kwa barua ya wazi iliyochapishwa kwenye tovuti rasmi ya Klabu ya Tottenham.
Daniel Levy ameeleza uamuzi wa kumtimua Ramos pamoja na Mkurugen

Washabiki wengi walikuwa wanamponda Mkurugenzi wa Michezo Damien Comoli kwa ushauri na shindikizo bovu la usajili wa Wachezaji. Damien Levy anajitetea: 'Katika miaka mitatu iliyopita tulitumia Pauni Milioni 175 kusajili Wachezaji kufuatia ushauri mbovu! Sasa tutamwachia masuala yote ya usajili Meneja Harry Redknapp ambae ataiarifu bodi chaguo lake la wachezaji anaowataka!'
Vilevile Mwenyekiti Levy aligusia kwa nini Robbie Keane na Dimitar Be

Levy anaongeza: 'Kwa ushauri wa Makocha tuliona Keane hawezi tena kukaa hapa Tottenham kwani ataleta kutoelewana. Tukakubali kumuuza.'
'Lakini Berbatov ni suala jingine! Levy aliendelea. 'Yeye alipofika tu hapa Tottenham msimu wa kwanza tu akataka ahamie Manchester United. Tulikataa lakini kila ukija wakati wa uhamisho aliendelea kudai kuhama. Tukaona atatuvuruga tukamuuza!'
Menyekiti huyo aliendelea utetezi wake kwa kuwajulisha Washabiki kuwa yeye daima anajali maslahi ya Tottenham na ameahidi ikifika Januari, wakati msimu wa uhamisho wa Wachezaji utakapofunguliwa tena, basi Meneja mpya Harry Redknapp atapewa fungu nono la kununua Wachezaji wapya.
No comments:
Post a Comment