Sunday 26 October 2008

Mwenyekiti wa Tottenham atetea uamuzi wa kumtimua Ramos na kumchukua Redknapp

Mwenyekiti wa Tottenham Hotspurs Daniel Levy [pichani kushoto akiwa na Ramos] ametoa utetezi wake kumfukuza kazi Meneja Juande Ramos kwa barua ya wazi iliyochapishwa kwenye tovuti rasmi ya Klabu ya Tottenham.
Daniel Levy ameeleza uamuzi wa kumtimua Ramos pamoja na Mkurugenzi wa Michezo Damien Comoli [pichani kulia Comoli na Ramos] na kumuajiri Meneja wa Portsmouth Harry Rednapp [pichani chini kulia] umefanywa ili klabu irudi katika utawala wa asilia wa klabu za soka Uingereza.
Washabiki wengi walikuwa wanamponda Mkurugenzi wa Michezo Damien Comoli kwa ushauri na shindikizo bovu la usajili wa Wachezaji. Damien Levy anajitetea: 'Katika miaka mitatu iliyopita tulitumia Pauni Milioni 175 kusajili Wachezaji kufuatia ushauri mbovu! Sasa tutamwachia masuala yote ya usajili Meneja Harry Redknapp ambae ataiarifu bodi chaguo lake la wachezaji anaowataka!'
Vilevile Mwenyekiti Levy aligusia kwa nini Robbie Keane na Dimitar Berbatov waliuzwa kwa kutamka kuwa Robbie Keane alitaka mwenyewe kwenda Liverpool kwa madai ni klabu aliyoipenda tangu yuko mdogo ingawa wao walitegemea angebaki Tottenham hadi anastaafu.
Levy anaongeza: 'Kwa ushauri wa Makocha tuliona Keane hawezi tena kukaa hapa Tottenham kwani ataleta kutoelewana. Tukakubali kumuuza.'
'Lakini Berbatov ni suala jingine! Levy aliendelea. 'Yeye alipofika tu hapa Tottenham msimu wa kwanza tu akataka ahamie Manchester United. Tulikataa lakini kila ukija wakati wa uhamisho aliendelea kudai kuhama. Tukaona atatuvuruga tukamuuza!'
Menyekiti huyo aliendelea utetezi wake kwa kuwajulisha Washabiki kuwa yeye daima anajali maslahi ya Tottenham na ameahidi ikifika Januari, wakati msimu wa uhamisho wa Wachezaji utakapofunguliwa tena, basi Meneja mpya Harry Redknapp atapewa fungu nono la kununua Wachezaji wapya.

No comments:

Powered By Blogger