Wednesday 29 October 2008

TONY ADAMS AWA MENEJA MPYA PORTSMOUTH

Tony Adams, mwenye umri wa miaka 42 na ambaye alikuwa Mchezaji wa zamani wa Arsenal na Timu ya Taifa ya Uingereza, ametangazwa kuwa ndie Meneja mpya wa Portsmouth kuchukua nafasi ya Harry Redknapp aliehamia Tottenham.
Kabla uteuzi huu Tony Adams alikuwa ndie Meneja msaidizi hapo hapo Portsmouth chini ya Harry Redknapp na alianza kazi hiyo mwaka 2006.
Tony Adams aliichezea Arsenal kama beki wa kati kuanzia mwaka 1983 hadi 2002 na alikuwa Mchezaji wa Timu ya Taifa ya Uingereza kuanzia 1987 hadi 2000 na alicheza mechi 66 zikiwemo Fainali za Kombe la Dunia mwaka 1998.

No comments:

Powered By Blogger