Monday 27 October 2008


KWA UFUPI TU TOKA LIGI KUU UINGEREZA:


Liverpool sasa inaongoza LIGI KUU kwa kuwa na pointi 23 kwa mechi 9 ilizocheza, Chelsea na Hull City ni za pili na za tatu zote zikiwa na pointi 20 kwa mechi 9 ingawa Chelsea iko mbele kwa magoli.
Ya nne ni Arsenal ikiwa na pointi 19 kwa mechi 9 ikifuatiwa na Aston Villa yenye pointi 17 kwa mechi 9.
Mabingwa Man U ni wa 6 wakiwa na pointi 15 kwa mechi 8, mechi moja pungufu kupita timu nyingine.
Mkiani wako Stoke nafasi ya 18 na wana pointi 7, Newcastle nafasi ya 19 kwa pointi 6 na wa mwisho ni Tottenham wana pointi 5.
Liverpool wameweza kuongoza ligi baada ya kuivunja ngome ya Chelsea walipowatwanga bao 1-0 nyumbani kwao Stamford Bridge ambako walikuwa hawajafungwa tokea Februari, 2004 na kwa mechi jumla ya mechi 86 za ligi.

Benitez ajigamba!

Meneja wa Liverpool Rafael Benitez amejigamba sasa kwamba kwa kuwa wameshazifunga Man U na Chelsea basi kila mtu ajue wao wanaweza kuchukua ubingwa.

Redknapp aanza vizuri!!!

Nae Harry Redknapp, Meneja mpya wa Tottenham, ameanza enzi yake mpya hapo Tottenham kwa kuipa klabu hiyo ushindi wake wa kwanza wa ligi msimu huu pale walipoifunga Bolton ba0 2-0.
Nayo klabu aliyotoka Rednapp, Portsmouth, imeanza ngwe bila ya Meneja huyo aliyeiwezesha klabu hiyo kunyakua Kombe la FA msimu uliopita, kwa sare ya 1-1 dhidi ya Fulham.

Robinho apachika 3!!

Robinho wa Man City alipachika mabao matatu mguuni kwake na kuiwezesha Man City kuifunga Stoke mabao 3-0.

Ronaldo kimwili na kiroho yuko Man U!!

Siku chache baada ya Rais wa Real Madrid Ramon Calderon kutamka klabu hiyo haina haja ya Ronaldo tena, Mchezaji huyo ameibuka na kusisitiza atabaki Manchester United kwa muda mrefu.
Ronaldo amekaririwa akisema: 'Sasa naelewa nimefanya uamuzi sahihi! Mie nipo Manchester kimwili na kiroho!

No comments:

Powered By Blogger