Saturday 25 October 2008

West Brom 0 Hull City 3

Hull City imeendeleza wimbi la kuwashangaza wengi kwa kushinda mechi tena ugenini na sasa kuwa nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi nyuma ya Chelsea na Liverpool na juu ya Arsenal na Man U.
Mabao matatu yalifungwa na Zayatte dakika ya 47, Geovanni dakika ya 62 na King ya 66.

Blackburn 1 Middlesbrough 1

Benny McCarthy, Mchezaji kutoka Afrika Kusini alieingizwa kipindi cha pili, ameiokoa timu yake Blackburn baada ya kusawazisha dakika za majeruhi kwa kichwa safi.

Afonso Alves aliipa Middlesbrough bao la kuongoza kwenye dakika ya 74.

No comments:

Powered By Blogger