Sunday 19 October 2008

MECHI ZA LEO: JUMAPILI, 19 Oktoba 2008

Hull City v West Ham [saa 11 jioni]

Stoke City v Tottenham [saa 12 jioni]

JUMATATU, 20 Oktoba 2008

Newcastle v Man City [saa 4 usiku]

REFA MSAIDIZI MECHI YA ASTON VILLA V PORTSMOUTH APASULIWA KICHWANI!!!

Katika mechi ya jana kati ya Aston Vill na Portsmouth iliyochezwa Villa Park nyumbani kwa Aston Villa na kuisha kwa sare ya 0-0 Refa Msaidizi, yaani mshika kibendera, aitwaye Phil Sharp, alirushiwa sarafu iliyompasua kichwani juu ya jicho la kulia na kumfanya aanguke chini kwa mstuko.
Pichani Refa mkuu kwenye mechi hiyo Mike Riley anaonekana akimpangusa jeraha msaidizi wake Phil Sharp.
Tukio hilo lilitokea dakika za mwisho mwisho za mchezo na ikabidi mechi isimame ili Refa huyo atibiwe na baada ya kubandikwa plasta Phil Sharp aliendelea kuchezesha.
Mtuhumiwa wa kosa hilo hakujulikana na Polisi wakishirikiana na Wana Usalama wa Uwanja wanachunguza kamera zinazochukua picha hapo uwanjani ili kumbaini mhalifu.
Klabu ya Aston Villa imetangaza wakimgundua huyo mtu basi hataruhusiwa tena kuingia Villa Park maishani mwake.

No comments:

Powered By Blogger