Wednesday 22 October 2008

MAN U NA ARSENAL ZAPETA UEFA CHAMPIONS LEAGUE!!!!

Timu za Uingereza Manchester United ambao ndio Mabingwa Watetezi wa UEFA CHAMPIONS LEAGUE na Arsenal jana zilipata ushindi murua katika mechi zao wakati Man U walipowabandika wapwa zao Celtic mabao 3-0 uwanjani kwake Old Trafford huku Arsenal akishinda ugenini Uturuki alipoichabanga Fenerbahce mabao 5-2.
Mabao ya Man U yaligungwa na Dimitar Berbatov mabao mawili na Wayne Rooney bao 1.
Wafungaji wa Arsenal walikuwa ni Adebayor, Walcott, Diaby, Song Billong na Ramsey.

Matokeo mengine ya mechi hizo za UEFA CHAMPIONS LEAGUE ni kama ifuatavyo:

Bayern Munich 3 Fiorentina 0

FC Porto 0 Dynamo Kiev 1

Juventus 2 Real Madrid 1

Steau Buchares 3 Lyon 5

Villareal 6 Aalborg 3

Zenit St Petrsburg 1 BATE Borisov 1

No comments:

Powered By Blogger