Wednesday 22 October 2008


DRO YA NCHI ZA AFRIKA KUELEKEA FAINALI KOMBE LA DUNIA 2010 YAFANYIKA MJINI ZURICH, USWISI

Nchi za Afrika 20 zilizofuzu kuingia hatua ya mwisho kutafuta wawakilishi wa Bara la Afrika katika FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA 2010 zitakazofanyika huko Afrika Kusini leo zimegawanywa katika Makundi matano ya Nchi 4 kila moja ambapo mshindi wa kila Kundi ndie atakaeingia FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA 2010 kujumuika na Mwenyeji wa mashindano Afrika Kusini.
Washindi watatu wa kwanza wa kila Kundi wataingia FAINALI ZA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA zitakazofanyika huko Angola pia mwaka 2010.

Mgawanyo wa MAKUNDI ni:

KUNDI A: Cameroun, Morocco, Gabon, Togo

KUNDI B: Nigeria, Tunisia, Kenya, Mozambique

KUNDI C: Egypt, Algeria, Zambia, Rwanda

KUNDI D: Ghana, Mali, Benin, Sudan

KUNDI E: Ivory Coast, Guinea, Burkina Faso, Malawi

No comments:

Powered By Blogger