Tuesday 21 October 2008

Newcastle 2 Manchester City 2

Manchester City ilijiokoa kutoka kipigo dhidi ya Timu iliyocheza na watu 10 tu kwa muda mrefu wa mchezo baada ya Beki wa Newcastle Habib Beye kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwenye dakika ya 13 tu ya mchezo baada ya Refa Rob Styles kudhani amemchezea rafu Robinho na pia kutoa penalti iliyofungwa na Robinho.
Tukio hilo liliwaudhi sana Newcastle kwani ilikuwa dhahiri sio penalti.
Shola Ameobi aliisawazishia Newcastle dakika ya 44.
Kipindi cha pili Beki wa Man City Richard Dunne alijifunga mwenyewe na kuwafanya Newcastle waongoze 2-1 hadi dakika ya 85 wakati Stephen Ireland aliposawazisha.
Newcastle: Given, Beye, Taylor, Coloccini, Bassong, Geremi, Guthrie, Butt, Duff, Martins (N'Zogbia 72), Ameobi (Carroll 79).AKIBA: Harper, Cacapa, Jose Enrique, Xisco, Edgar.
Man City: Hart, Richards (Onuoha 58), Ben-Haim, Dunne, Garrido (Sturridge 83), Wright-Phillips, Kompany, Hamann (Evans 64), Ireland, Jo, Robinho.AKIBA: Schmeichel, Elano, Fernandes, Berti.
WATAZAMAJI: 45,908

No comments:

Powered By Blogger