Wednesday 22 October 2008

BECKHAM AJIUNGA AC MILAN KWA MKOPO

Nyota wa Uingereza David Beckham, miaka 33, atajiunga na Klabu ya Italia AC Milan kwa mkopo kuanzia Januari mwakani hadi mwisho wa msimu huu.
Kwa sasa Beckham ni Mchezaji wa Klabu ya Los Angeles Galaxy ya Marekani ambao msimu wao wa ligi unakwisha wikiendi hii na kuanza msimu mpya ni mpaka Aprili mwakani na hii inamaanisha Beckham angekuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu hivyo kuhatarisha hata uteuzi wake kwenye Timu ya Taifa ya Uingereza.
Beckham anahitaji achezee Timu ya Taifa ya Uingereza mechi mbili tu zaidi ili avunje rekodi ya Bobby Moore aliyochezea mechi 108 ingawa rekodi ya mechi nyingi inashikiliwa na Kipa Peter Shilton aliecheza mechi 128.
Akiwa AC Milan atajiunga na mastaa wa Brazil kama Ronaldinho, Kaka na Alexandre Pato pamoja na wa Italy kama Andrea Pirlo na Gennaro Gattuso.

No comments:

Powered By Blogger