Friday 24 October 2008

FA YAIFUTA KADI NYEKUNDU YA BEYE WA NEWCASTLE

Kamati ya Sheria ya FA leo imeifuta kadi nyekundu aliyopewa Beki wa Newcastle Habib Beye kwenye dakika 13 tu ya mchezo na Manchester City na Refa Rob Styles ambae pia alitoa penalti iliyofungwa na Robinho.
Katika mechi hiyo, Newcastle waliocheza watu 10 tangu dakika hiyo ya 13 walitoka suluhu ya 2-2 na Manchester City.
Hii inamaanisha adhabu ya kufungiwa ya kutocheza mechi moja ya Mchezaji huyo raia wa Senegal nayo pia imeondolewa.
Marudio ya video yalidhihirisha Habib Beye alicheza mpira na hakumchezea faulo Robinho [pichani].
Hii ina maana Beye yuko huru kucheza mechi ya Jumamosi wakati Newcastle watakapopambana na Sunderland.

No comments:

Powered By Blogger