Saturday 17 January 2009

Dunia yashangazwa na Dau la kumnunua Kaka kutoka AC Milan kwenda Man City!!!!
NI ZAIDI YA PAUNI MILIONI 100!!!

Nia ya Klabu ya Manchester City kutaka kumnunua Kaka kwa Pauni Milioni 100 na kumlipa Mshahara wa Pauni Laki 500 kwa wiki, zote zitakuwa ni rekodi za dunia kwa mbali kabisa, imewashangaza wadau wengi wa soka huko Ulaya.
Angalia watu muhimu wanavyochukulia taarifa hizo za uhamisho wa Kaka.
-Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson:
'Inakuwa ngumu kwangu kuelewa hilo! Inashangaza lakini soka ni soka na wakati mwingine unapata mistuko na maajabu na hili lazima limemshangaza kila mtu! Sidhani kama uhamisho huu utatudhuru sisi lakini hilo dau halieleweki!'
-Meneja wa Arsenal Arsene Wenger:
'Sijiskii wala sihisi kama Man City wako dunia hii kwa sababu sisi tuko kwenye klabu ya soka iliyo kwenye dunia ya kikweli. Uhamisho huu utaleta madhara makubwa kwenye soko la uhamisho wa Wachezaji. Utapandisha bei wakati kote duniani bei zinaporomoka! Sisi tupo kwenye dunia ya soka inayotegemea mapato yake yote kutoka kwa viingilio mlangoni, wadhamini wa matangazo na mapato kwenye matangazo ya TV!'

-Meneja wa AC Milan Carlo Ancelotti:
'Tegemeo langu ni kumfundisha Kaka kwa miaka mingi zaidi lakini lazima tukubali ukweli na tathmini iliyofanya AC Milan kwenye dau lilopendekezwa! Nadhani kuna makubaliano klabu itafanya pamoja na Kaka. Lakini nia yetu siku zote, tuwe na Kaka au tusiwe nae, ni kushindana na kushinda.'
-Alan Shearer, Mchezaji wa zamani wa England:
'Tunazungumzia Mchezaji Bora duniani lakini huwezi kuniambia yeye ana thamani hiyo! Dau hilo ni kitu hakijawahi kuonekana! Kwangu mimi, medali ni kitu muhimu kuliko pesa kwa Mchezaji!
Huwezi kuniambia Robinho ameenda Manchester City kupata medali kwani timu hiyo haiwezi kushinda chochote! Nadhani yuko huko kufuata pesa tu!!'
-Scolari wa Chelsea:
'Hii ni soka na Kaka ni Mchezaji wa kulipwa! Labda wanataka Man City iwe Klabu kubwa.'
-Clarence Seedorf, Mchezaji mwenzake Kaka huko AC Milan:
'Hilo dau ni kama sinema ya Hollywood! Pengine Man City wanatuma ujumbe kuionyesha dunia wanataka kuwa klabu kubwa duniani!'
-Rodney Marsh, Mchezaji staa wa zamani Man City:
'Inastusha! Ni dili kubwa sana, sana!! Lakini swali kubwa ni je hii itaisaidia Man City kuwa Timu bora LIGI KUU? Sidhani hata chembe!!!!'

SCOLARI: 'Ntawauza wote!!'

Meneja wa Chelsea Luiz Felipe Scolari amembwaga Didier Drogba nje ya kikosi chake kinachocheza leo nyumbani Stamford Bridge na Stoke City kwenye ya mechi ya LIGI KUU na pia kumwambia hata asikanyage uwanjani hapo.
Mbali ya kumtema Drogba kwa mechi mbili mfululizo ya kwanza ikiwa ile ya Jumatano Chelsea walipocheza ugenini na Southend na kushinda 4-1 katika mechi ya mashindano ya Kombe la FA, Scolari amewatisha Wachezaji wake wote na kuwaambia anaetaka kuhama hii ni nafasi yake kabla dirisha la uhamisho halijafungwa mwishoni mwa Januari.
Msimamo huu mkali wa Scolari unafuatia kipigo kitakatifu walichoangushiwa Chelsea Jumapili iliyopita na Mabingwa Manchester United waliposhindiliwa mabao 3-0.
Scolari alibwaka: 'Huu ni wakati wa kila Mchezaji kucheza kitimu, kwa moyo na mapenzi kwa Chelsea. Huwezi ondoka klabu, badilisha, nafasi iko wazi mpaka mwisho wa mwezi!'

No comments:

Powered By Blogger