Thursday 15 January 2009

KWA UFUPI:
-Man City waendelea kumsaka Kaka!

Klabu ya Manchester City kupitia Meneja wao Mark Hughes wamesema bado wana nia ya kumchukua staa wa Brazil Kaka kutoka AC Milan ya Italia na mazungumzo bado yanaendelea ingawa uamuzi haujafikiwa.
Inasemekana dau la kumuhamisha Kaka litazidi Pauni Milioni 100 na hii itakuwa rekodi ya dunia kwa uhamisho.

-Drogba bado anahitajika Chelsea

Meneja msaidizi wa Chelsea Ray Wilkins amesema Klabu ya Chelsea bado inamhitaji Didier Drogba na hatua ya kumtema jana kwenye kikosi kilichoenda kucheza mechi ya Kombe la FA na Southend ambako waliibuka na ushindi wa mabao 4-1 ni uamuzi wa Meneja Luiz Felipe Scolari wa kubadilisha Wachezaji na wala si hatua ya kumwondoa Chelsea.
Hivi karibuni kumekuwa na tetesi nzito kwamba Drogba ataenda Italia kuungana na aliekuwa Meneja wa Chelsea Jose Mourinho ambae kwa sasa yuko Inter Milan.

-Wenger bado ana matumaini ya kumsaini Arshavin

Arsene Wenger wa Arsenal ametamka kuwa majadiliano bado yanaendelea na Klabu ya Kirusi Zenit St Petrsburg ya kumsaini nyota wa Urusi Andrei Arshavin.
Wenger alisema: 'Pengine si leo ila tunazungumza na ikiwezekana sawa isipowezekana basi! Hatuwezi kukiuka misimamo yetu!'

-Rooney nje wiki 3!!

Nyota wa Mabingwa Manchester United Wayne Rooney anategemewa kuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki kama 3 baada ya kuumia mara tu baada ya kufunga bao la ushindi kwenye mechi ya jana ya LIGI KUU dhidi ya Wigan iliyochezwa Old Trafford.
Rooney alifunga bao hilo kwenye sekunde ya 53 tu ya mchezo na akatoka nje ya uwanja dakika ya 6 tu ya mchezo.
Ikiwa atakuwa nje wiki hizo 3 basi Rooney atazikosa mechi zijazo dhidi ya Bolton [LIGI KUU], Derby [CARLING CUP], Tottenham [FA CUP], West Bromwich na Everton [zote za LIGI KUU].

MECHI ZIJAZO ZA LIGI KUU: [saa za kibongo]

Jumamosi, 17 Januari 2009
[saa 12 jioni]
Blackburn v Newcastle]
Bolton v Man U
Chelsea v Stoke
Man City v Wigan
Sunderland v Aston Villa
West Brom v Middlesbrough
[saa 2 na nusu usiku]
Hull v Arsenal
Jumapili, 18 Januari 2009
[saa 10 na nusu jioni]
West Ham v Fulham
Tottenham v Portsmouth
Jumatatu, 19 Januari 2009
[saa 5 usiku]
Liverpool v Everton

No comments:

Powered By Blogger