Saturday 17 January 2009

MABINGWA Man U waongoza LIGI KUU kwa mara ya kwanza msimu huu!!

Manchester United, Mabingwa Watetezi wa LIGI KUU England, wakicheza ugenini na Bolton Wanderers walishinda kwa goli la dakika ya 90 lililofungwa na Dimitar Berbatov na kuwafanya waongoze kwa mara ya kwanza tangu msimu uanze.
Man U wako na pointi 47 kwa mechi 21 wakifuatiwa na Liverpool pointi 46 mechi 21 na watatu ni Chelsea pointi 45 mechi 22, Aston Villa pointi 44 mechi 22 na watano Arsenal pointi 41 mechi 22.
Liverpool anacheza Jumatatu saa 5 usiku [bongo taimu] na Watani wake wa jadi watoto wa mji mmoja Liverpool, Timu ya Everton na mechi hii haitabiriki.
Na hata Liverpool akishinda mechi hiyo atakuwa mbele ya Manchester United kwa sababu ya kucheza mechi moja mbele.

MATOKEO KAMILI:
Bolton 0 v Man U 1
Chelsea 2 v Stoke 1
Man City 1 v Wigan 0
Sunderland 1 v Aston Villa 2
West Brom 3 v Middlesbrough 0
Hull 1 v Arsenal 3

No comments:

Powered By Blogger