Sunday 11 January 2009

Mabingwa Man U wawashindilia Chelsea!

Chelsea walipata kipigo kitakatifu ndani ya Old Trafford baada ya kubamizwa magoli 3-0 na Mabingwa wa England, Ulaya na Dunia Manchester United.
Kwenye mechi ambayo magazeti ya Uingereza yaliwekea bango kauli za ajabu za Meneja wa Liverpool Rafa Benitez za kumshambulia Sir Alex Ferguson ambae hakujibu chochote, sasa majibu yametoka Uwanjani!
Msimu wote huu Chelsea hawajahi kufungwa ugenini na leo kilikuwa kipigo chao cha kwanza.
Goli la kwanza la Man U lilifungwa na Vidic baada ya kona ya Giggs.
La pili alifunga Rooney kufuatia gonga murua kati ya Ronaldo na Evra kwenye wingi ya kushoto.
Berbatov alipachika bao la 3 kufuatia frikiki safi ya Ronaldo.
TIMU ZILIKUWA:
Man Utd: Van der Sar, Neville, Vidic, Evans, Evra (O'Shea 66), Ronaldo, Fletcher, Giggs (Carrick 79), Park, Berbatov, Rooney.
Akiba hawakucheza: Kuszczak, Anderson, Scholes, Welbeck, Tevez.
Kadi: Ronaldo, Rooney, Park.
Magoli: Vidic 45, Rooney 63, Berbatov 87.
Chelsea: Cech, Bosingwa (Belletti 64), Carvalho, Terry, Ashley Cole, Mikel, Joe Cole (Di Santo 85), Lampard, Ballack, Deco (Anelka 46), Drogba.
Akiba hawakucheza: Cudicini, Ivanovic, Ferreira, Kalou.
Kadi: Lampard, Bosingwa, Carvalho, Terry, Belletti.
Watazamaji: 75,455
Refa: Howard Webb

No comments:

Powered By Blogger