Monday 12 January 2009

Sclorari: 'Kipigo kimetuumiza!'

Meneja wa Chelsea, Luis Felipe Scolari, amekiri kipigo cha 3-0 walichokipata Old Trafford kutoka kwa Mabingwa Manchester United kimewaumiza vibaya ingawa bado anadai lolote linaweza kutokea kwani wamebakiza mechi 17.
'Manchester United walikuwa bora kupita sisi!' Scolari alikiri 'Lakini sasa ni wakati wa kufikiria nini cha baadae, inabidi tujikaze kama wanaume na tuwe bora zaidi.'

Ferguson: 'Benitez ni mpuuzi!'

Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, amemwita Meneja wa Liverpool Rafa Benitez mpuuzi kufuatia tuhuma dhidi yake.
Ferguson, aliehojiwa jana na Waandishi wa Habari, hakutaka kuingia ndani juu ya tuhuma hizo na alijibu kifupi: 'Maneno yake yalikuwa na sumu kali! Lakini akikaa chini na kutafakari atajiona ni mpuuzi! Nadhani ni mtu mwenye hasira! Kuna kitu kinamsumbua!'

Wenger asikitishwa na mbinu za Timu za LIGI KUU

Arsene Wenger, Meneja wa Arsenal, anakerwa sana na mbinu za Timu za LIGI KUU za kujihami kwa kupindukia.
Juzi Arsenal ilibidi wasubiri hadi dakika ya 84 ili wapate bao la ushindi lililofungwa na Bendtner dhidi ya Bolton waliocheza defensi ya watu 10 muda wote wa mchezo.
Wenger alisema: 'Miaka 10 iliyopita nilipofika hapa England kila timu ilicheza 4-4-2 lakini sasa ni timu chache sana zinakuja kucheza na Washambuliaji wawili! Kila timu inajihami na hata hao Manchester United wenye Washambuliaji hodari wanapata taabu kufunga! Lakini mbinu hizo za kujihami zitashindwa tu kwani sasa wanatufanya tutilie mkazo mbinu za kuwa na wepesi wa kubadili nafasi kwa haraka, ubunifu na kasi ya mchezo!'

No comments:

Powered By Blogger