Wednesday 14 January 2009

MECHI ZA LEO England

Jumatano, 14 Januari 2009 [saa za bongo]


LIGI KUU England


Man U v Wigan [saa 5 usiku]

FA Cup [Marudiano]

Crystal Palace v Leicester [saa 5 usiku]

Newcastle v Hull [saa 4 dak 45 usiku]

Southend v Chelsea [saa 5 dak 10 usiku]

Matokeo mechi za jana za Kombe la FA

Birmingham 0-2 Wolverhampton

Bristol City 0-2 Portsmouth

Burnley 2-1 QPR [baada ya dakika za nyongeza 30]

Cheltenham 0-0 Doncaster

Crew 2-3 Millwall

Histon 1-2 Swansea

LeytonOrient 1-4 Sheffield United

Norwich 0-1 Charlton

Peterborough 0-2 West Brom

HABARI KWA UFUPI:

Evra kuwa nje kwa wiki 4!

Patrice Evra, beki mahiri wa Man u, atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki 3 au 4 baada ya kuumia mguu wakati akipiga krosi iliyomuunganisha Rooney aliefunga bao la pili katika ushindi wa 3-0 wa Man U dhidi ya Chelsea siku ya Jumapili iliyopita.

Man City wapo katika mazungumzo na AC Milan ili wamnunue Kaka!

Taarifa zisizothibitishwa zinadai Manchester City ipo mbioni kumnunua Kaka kutoka kwa AC Milan kwa kitita kitakachovunja kila aina ya rekodi. Inadaiwa dau la ununuzi ni Pauni Milioni 100 na Mshahara wake utakuwa Pauni Laki 5 kwa wiki!!

Mabingwa Watetezi wa Kombe la FA Portsmouth waingia Raundi ya 4!!

Bao tata la Straika Peter Crouch na lingine la Niko Kranjcar limeipa ushindi Portsmouth ambao ndio Mabingwa wa FA Cup msimu uliopita wa 2-0 hapo jana walipocheza na Timu ya Daraja la chini Bristol City.

Mkurugenzi Mtendaji wa Man U David Gill amkandya Benitez!!

Davidi Gill, Mkurugenzi Mtendaji wa Man U na ambae pia ni mmoja wa viongozi wa juu wa FA, ameziita kauli za Meneja wa Liverpool zilizohoji kuwepo kwake FA ni za kupotosha na kuficha ukweli.

Benitez alimkurupukia Gill mara tu baada ya kumwandama Sir Alex Ferguson ambae alijibu mapigo kwa mkato pale alipombandika jina la 'mpuuzi' Benitez.

David Gill amesema kuwapo kwake pale FA ni baada ya kuchaguliwa na Klabu zote za LIGI KUU na ndio taratibu za England za wao kusimamia masuala ya kibiashara na mapato huku Kamati mbalimbali zikiiendesha FA katika shughuli zake za kila siku na haziingiliwa hata chembe na wao.

David Gill yeye ni mmoja tu wa viongozi wa FA ambao wanatoka na waliwahi kutoka Klabu kadhaa za LIGI KUU.


No comments:

Powered By Blogger