Thursday 15 January 2009

Man United wapaa na kushika nafasi ya pili, pointi 2 nyuma ya Liverpool, mechi moja mkononi!!

Mabingwa watetezi wa LIGI KUU England Manchester United wamewafunga Wigan goli 1-0 goli lililofungwa na Wayne Rooney sekunde ya 53 tu tangu mechi ianze baada ya pasi yenye akili toka kwa Mchezaji Bora Duniani Cristiano Ronaldo.
Rooney hakucheza muda mrefu baada ya hapo kwani alitolewa dakika ya 6 ya mchezo baada ya kupata maumivu.
Sasa Manchester United wako nafasi ya pili katika msimamo wa LIGI KUU England wakiwa na pointi 44 baada ya kucheza mechi 20.
Vinara Liverpool wana pointi 46 kwa mechi 21.
Timu ya tatu ni Chelsea wana pointi 42 kwa mechi 21 na Aston Villa ni wanne wakiwa na pointi 41 kwa mechi 21.
Arsenal ni wa tano wakiwa na pointi 38 kwa mechi 21.
Manchester United wanacheza ugenini na Bolton Wanderers siku ya Jumamosi inayokuja na endapo watashinda mechi hiyo watachukua uongozi wa LIGI KUU kwani Liverpool anacheza Jumatatu na watani wake wa jadi wenzake wa mji mmoja, mji wa Liverpool, Klabu iitwayo Everton.
Hii ni mechi isiyotabirika.

MATOKEO MECHI ZA FA CUP:

Southend 1 Chelsea 4

Newcastle 0 Hull City 1

Crystal Palace 2 Leicester 1

No comments:

Powered By Blogger