Tuesday 13 January 2009

Fernando Torres: 'Man U watashinda LIGI KUU!.............Na Meneja wake Benitez sasa amgeukia Mkurugenzi wa Man U!!!

Wakati Mchezaji nyota wa Liverpool, Fernando Torres anakiri Manchester United wana nafasi nzuri kutetea vyema taji lao la Ubingwa wa LIGI KUU England, Meneja wake Rafa Benitez ambae alimshambulia Sir Alex Ferguson hivi juzi tu, sasa ameelekeza mtutu kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Manchester United, David Gill, ambae pia ni mmoja wa viongozi wa FA, Chama cha Soka cha England.
Torres alikaririwa akisema: 'Man U wana nafasi kubwa, ni timu bora, ngumu na kwa miaka mingi wameonyesha wako madhubuti sana! Tena wana mechi mbili mkononi!'
Torres anakiri kuwa mechi kati ya Manchester United na Liverpool itakayochezwa Old Trafford Machi 14 ndio itatoa mwelekeo nani Bingwa.
Wakati huohuo, Meneja wake Rafa Benitez ameendelea kuishambulia Manchester United na safari hii amempiga kwanja mtendaji wa juu wa Klabu hiyo David Gill ambae ni Mkurugenzi Mtendaji wa Man U na vilevile ana wadhifa kwenye FA kwa kuhoji kuweko kwake kwenye FA.
Ni kawaida kwa viongozi wa Klabu huko England vilevile kushika nyadhifa kwenye FA na hasa wakisimamia upande wa biashara, mapato na mgawanyo wa mapato hasa urushaji matangazo kwenye TV.
Kwa miaka kadhaa hapo nyuma, David Dean aliekuwa Makamu Mwenyekiti wa Arsenal alikuwa kiongozi wa juu huko FA.
Sir Alex Ferguson alijibu shutuma dhidi yake kwa kuziita ni upuuzi.

Stoke wamsaini James Beattie.

Timu ya Stoke City imemchukua Mshambuliaji James Beattie kutoka Timu ya Daraja la chini Sheffield United kwa dau la Pauni Milioni 3 na nusu na kwa mkataba wa miaka miwili na nusu.
James Beattie, mwenye miaka 30, aliwahi kuchezea LIGI KUU akiwa na Timu ya Southampton.

No comments:

Powered By Blogger