Wednesday 14 January 2009

Wakati Benitez arudi hospitali kwa operesheni, David Gill amshushua!!!

Meneja wa Liverpool, Rafa Benitez, alietumia wiki yote iliyokwisha kwa kuishambulia Manchester United alipodai Sir Alex Ferguson 'anaua' Marefa na haadhibiwi na kisha kumrukia Mkurugenzi Mtendaji wa Manchester United David Gill ambae pia yuko kwenye Bodi ya FA, Chama cha Soka England, na kudai Manchester United wanamiliki kila kitu, amerudishwa tena hospitali kufanyiwa operesheni ya tatu ili kuondoa vijiwe kwenye figo zake.
Mwezi Desemba, 2008 alifanyiwa operesheni kwa tatizo hilohilo.
Baada ya kuanza kumshambulia Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson alijibu kwa ufupi na kusema: 'Ni upuuzi! Huyu ni mtu mwenye hasira! Nadhani kuna kitu kinamsumbua!'
David Gill, Mkurugenzi Mtendaji wa Manchester United, akiwa ziarani Mashariki ya Mbali huko Macau, alijibu tuhuma za Benitez kwa kueleza: 'Kauli za Benitez hazina ukweli hata chembe! Ukweli ni kwamba kwenye Bodi ya FA kuna Wawakilishi Watatu wa Klabu za LIGI KUU-yuko Mwenyekiti Dave Richards, yupo Mwenyekiti wa Klabu ya Bolton Wanderers Phil Gartside na mimi. Sote tunachaguliwa kila mwaka na Klabu zote za LIGI KUU ikiwemo Liverpool! Mimi nipo Bodi hiyo huu ukiwa mwaka wa pili na nikiwa kule siwakilishi Manchester United bali Klabu zote za LIGI KUU!!'
Gill akamalizia: 'Ukitazama ukweli kuhusu maamuzi ya FA na kila kitu kinachoihusu Manchester United utaona hamna upendeleo na badala yake ni tofauti! Huyu anatushangaza wote!!'

Refa Howard Webb aomba msamaha kwa kusaidia kufunga goli!!

Refa Howard Webb [pichani] ambae sasa anasifika ndie bora na juzi Jumapili ndie aliechezesha 'BIGI MECHI' kati ya Manchester United na Chelsea ambapo Man U waliibuka kidedea kwa bao 3-0, jana alichezesha mechi ya Kombe la FA kati ya Birmingham na Wolves ambayo Wolves walishinda ugenini bao 2-0.
Lakini, Refa Howard Webb ilibidi aombe msamaha kwa Klabu ya Birmingham baada ya kutibua pasi ya Radhi Jaidi wa Birmingham iliyomgonga kwa bahati mbaya na kumkuta Mshambuliaji wa Wolves Andy Keogh aliempasia Sam Vokes aliepachika bao la pili.
Howard Webb alisikitika: 'Sikufurahia na niliwaomba msamaha Birmingham! Walinielewa!'
Sheria za Soka hazimlazimshi Refa kusimamisha mechi endapo mpira unamgusa.

No comments:

Powered By Blogger