Friday 15 May 2009

RATIBA LIGI KUU ENGLAND:

Jumamosi, 16 Mei 2009
[saa 8 dak 45 mchana]
Man U v Arsenal
[saa 11 jioni]
Bolton v Hull
Everton v West Ham
Middlesbrough v Aston Villa
Newcastle v Fulham
Stoke v Wigan
Tottenham v Man City
Jumapili, 17 Mei 2009
[saa 9 na nusu mchana]
West Brom v Liverpool
[saa 12 jioni]
Chelsea v Blackburn
Jumatatu, 18 Mei 2009
[saa 4 usiku]
Portsmouth v Sunderland

Wenger awaomba Mashabiki kuwa wavumilivu!
Arsene Wenger, Meneja wa Arsenal, amewataka wadau wa Arsenal kuvumilia wakati akiijenga Timu mpya na amekubali kuwajibika ikiwa katika mwaka mmoja au miwili ijayo mikakati yake haifanikiwi.
Arsenal tangu mwaka 2005 walipoifunga Manchester United kwa matuta na kuchukua FA CUP hawajachukua Kombe lolote jingine.
Wenger alipata wakati mgumu sana alipokutana na Wadau wa Arsenal ambao walimshambulia kwa maswali kadha wa kadhaa. Lakini, kama alivyobatizwa 'Profesa' aliyapanchi vizuri na kusisitiza ana kikosi cha chipukizi na ataongeza nguvu pale panapo hitajika.
NAHODHA WA ASTON VILLA LAURSEN ASTAAFU SOKA!!

Nahodha wa Klabu ya Aston Villa Martin Laursen kutoka Denmark amelazimika kustaafu kucheza soka baada ya kuumia goti.
Lursen, miaka 31, amekuwa akipata matatizo ya mara kwa mara ya goti na mara ya mwisho aliumia mwezi Desemba.

No comments:

Powered By Blogger