Tuesday 12 May 2009

VIOJA VYA SOKA!!!!!
Duniani kuna vituko na mikasa mingi na hata Dunia ya Soka haikosi vibweka vyake!!!

Angalia kushoto ni bango la tahadhari ambalo kawaida huwekwa wakati sakafu inapigwa deki ili kumtahadharisha mtu asiteleze lakini Mdau mmoja amelibadilisha na kutoa tahadhari jinsi Wachezaji wa Italia walivyo Mabingwa kwa kujidondosha makusudi!!!!


Mdau hana Wapinzani wa kusakata nao kabumbu lakini Ng'ombe anao!!!! Akajikita Kiwanjani kuwapiga chenga Ng'ombe zake!!!
Yote ni starehe na burudani ya Soka!!!!


Wadau hawana Kiwanja cha Mpira lakini hawakukata tamaaaa!!!!! Wakaenda kando ya Ziwa kwenye kilima na kujitengenezea 'NESHNO STEDIUMU' yao burudani huku imepambwa na 'pori' la mimea mikubwa!!!!
Bila shaka Timu yenye Kiwanja hiki 'spesho' wakiingia kwenye Viwanja vya kawaida vilivyo tambarare basi soka lao litakuwa la kutisha sana maana mazoezi wanayoyapata kwenye Kiwanja hiki kilicho chini juu ni magumu sana na bora sana!!!!
Wachezaji wakilala yombo ovyo basi wanaishia Ziwani!!!!

No comments:

Powered By Blogger