Saturday 16 May 2009

BINGWA KAPATIKANA ILA KIMBEMBE NANI ANASHUSHWA DARAJA?

Wakati leo Manchester United amenyakua Ubingwa wa LIGI KUU England, Hull City kajichomoa toka eneo la hatari la kushuka Daraja na kumrudisha Newcastle katika eneo hilo, Middlesbrough ndio anachungulia kushushwa pamoja na West Bromwich!

Hull City akicheza ugenini Reebok Stadium ametoka suluhu na Bolton ya bao 1-1 na anaweza kupona kwenye mechi yake ya mwisho atakapowakaribisha Mabingwa Manchester United kwake KC Stadium kwenye mechi ya mwisho ya ligi.

Middlesbrough yuko kwenye mashaka makubwa baada ya kutoka sare 1-1 na Aston Villa na bado wako nafasi ya pili toka mkiani na hata wakishinda mechi yao ya mwisho bado wanahitaji wengine wawasaidie ili wapone.

Newcastle wakiwa nyumbani walifungwa 1-0 na Fulham na sasa wameporoka kwenda nafasi ya 18. Mechi yao ya mwisho ni ya ugenini watakapocheza na Aston Villa.

Msimamo kwa Timu za chini ni: [TIMU ZILIZO NAFASI YA 18 HADI 20 NDIZO HUSHUSHWA]

-Nafasi ya 13: Bolton pointi 41

-Nafasi ya 14: Blackburn pointi 40

-Nafasi ya 15: Portsmouth pointi 38

-Nafasi ya 16: Sunderland pointi 36

-Nafasi ya 17: Hull City pointi 35

-Nafasi ya 18: Newcastle pointi 34

-Nafasi ya 19: Middlesbrough pointi 32

-Nafasi ya 20: West Brom pointi 31

No comments:

Powered By Blogger