Sunday 17 May 2009

Real atwangwa Barcelona atwaa Ubingwa!!!!
AC Milan afungwa, Inter Milan atwaa Ubingwa!!!

Baada ya kuchapwa mabao 3-2 na Villareal, Real Madrid wameupeleka Ubingwa wa Spain kwa Watani wao wa Jadi Barcelona ambao jana hawakucheza.
Ubingwa huu ni wa 19 kwa Barcelona ambao wiki iliyopita pia walishinda Kombe la Mfalme Spain kwa kuifunga Atletic Bilbao 4-1.
Barcelona watacheza Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE hapo Mei 27 mjini Rome, Italia na Mabingwa wa Watetezi wa Ulaya Manchester United ambao jana walitwaa kwa mara ya 18 Ubingwa wa England.

Huko Italia, mambo yalikuwa kama Spain pale AC Milan, Klabu yenye uhasama na na Inter Milan, ilipopigwa 2-1 na Udinese hapo jana na kuwazawadia mahasimu wao Inter Milan Ubingwa wa Italia wa ligi ya Serie A bila ya Inter Milan kuwa na mechi jana.
Mara baada ya mechi hiyo ya Udinese na AC Milan kwisha, mashabiki wa Inter Milan [pichani] walifurika katikati ya jiji la Milan kusheherekea ushindi wao.
Inter Milan, wanaoongozwa na Meneja wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho, sasa wametwaa 'SCUDETTO' kwa mara ya 4 mfululizo.

No comments:

Powered By Blogger