Sunday 17 May 2009

BINGWA KAPATIKANA SASA LIVERPOOL NA CHELSEA WAGOMBEA NAFASI YA 2!!!

Baada ya vita kati ya Manchester United na Liverpool kumalizika rasmi jana kwa Manchester United kuchukua Kombe la Ubingwa wa LIGI KUU England, sasa Liverpool yuko kwenye vita yake nyingine ya kuhakikisha anamaliza nafasi ya 2 mbele ya Chelsea. Liverpool yuko nafasi ya 2 na ana pointi 80 na Chelsea ni wa 3 akiwa na pointi 77 huku Timu zote zimebakisha mechi 2.
Leo Liverpool mgeni wa West Bromwich ambao wako kwenye balaa la kushushwa Daraja wakiwa wako mkiani na Chelsea yuko kwake Stamford Bridge kucheza na Blackburn ambayo matokeo ya mechi za jana yamemhakikishia yuko salama LIGI KUU.
RATIBA LIGI KUU ENGLAND-LEO NA KESHO:
Jumapili, 17 Mei 2009
[saa 9 na nusu mchana]
West Brom v Liverpool
[saa 12 jioni]
Chelsea v Blackburn
Jumatatu, 18 Mei 2009
[saa 4 usiku]
Portsmouth v Sunderland
MATOKEO KAMILI MECHI ZA JANA:
Jumamosi, 16 Mei 2009
Man U 0 v Arsenal 0
Bolton 1 v Hull 1
Everton 3 v West Ham 1
Middlesbrough 1 v Aston Villa 1
Newcastle 0 v Fulham 1
Stoke 2 v Wigan 0
Tottenham 2 v Man City 1

No comments:

Powered By Blogger