Saturday 23 May 2009

BUNDESLIGA: MWISHO LEO!!!! BINGWA NANI?

Ligi ya Ujerumani inaisha leo jioni kwa Timu zote kucheza mechi zao za mwisho kuanzia saa 10 na nusu, bongo taimu, na, ingawa Wolfsburg yuko kileleni akiwa na pointi 66 nyuma yake ipo Timu Kongwe Bayern Munich na pia Vfb Stuttgart, waliofungana pointi 64 huku Hertha Berlin wakishika nafasi ya 4 wakiwa na pointi 63. Vinara Wolfburg wanahitaji suluhu tu wachukue Ubingwa huku Bayern Munich na Vfb Stuttgart, wanaokutana pamoja, inabidi kwanza wapate ushindi na pili waombee matokeo mabaya kwa Wolfsburg.

MECHI ZA LEO ZA VINARA:

Bayern Munich v VfB Stuttgart,
Wolfsburg v Werder Bremen,
Karlsruhe v Hertha Berlin,

No comments:

Powered By Blogger