Thursday 21 May 2009

KOMBE LA MWISHO LA UEFA LAENDA UKRAINE:

Shakhtar Donetsk 2 Werder Bremen 1


Bao la muda wa nyongeza la Rodrigues Jadson liliwalaza Werder Bremen ya Ujerumani na kuhakikisha Shakhtar Donetsk ya Ukraine wanaondoka na Kombe la UEFA ambalo ni la mwisho kushindaniwa kwani msimu ujao mashindano haya yataitwa UEFA EUROPA LEAGUE. Fainali hii ilichezwa Istanbul, Uturuki Uwanja wa Sukru Saracoglu ambao ni mali ya Klabu maarufu ya huko Uturuki Fernebahce.
Luiz Adriano aliifungia Shakhtar bao la kwanza dakika ya 25 lakini Werder Bremen wakasawazisha kabla ya hafutaimu mfungaji akiwa Ronaldo Naldo kwa frikiki ya mbali ambayo Kipa wa Shaktar Andriy Pyatov aliisindikiza wavuni.
Timu hizi zilikuwa 1-1 hadi mwisho wa dakika 90 ndipo ukaingia muda wa nyongeza wa dakika 30 na dakika 7 tu toka muda wa nyongeza uanze Shakhtar wakapata bao lao la ushindi.
Vikosi vilikuwa:
Shakhtar Donetsk: Pyatov, Srna, Kucher, Chigrinsky, Rat, Lewandowski, Fernandinho, Ilsinho (Gai 99), Jadson (Duljaj 112), Willian , Luiz Adriano (Gladkyy 89). Akiba hawakucheza: Khudzamov, Ischenko, Chyzhov, Moreno.
Kadi: Srna, Lewandowski, Ilsinho.
Magoli: Luiz Adriano 25, Jadson 97.
Werder Bremen: Wiese, Fritz (Pasanen 94), Prodl, Naldo, Boenisch, Niemeyer (Tziolis 103), Frings, Baumann, Ozil, Pizarro, Rosenberg (Hunt 78). Akiba hawakucheza: Vander, Tosic, Vranjes, Harnik.
Kadi: Frings, Fritz, Tziolis, Boenisch.
Goli: Naldo 35.
Watazamaji: 53,100.
Refa: Luis Medina Cantalejo (Spain).

No comments:

Powered By Blogger