Tuesday 19 May 2009

Sunderland wafungwa na Portsmouth 3-1, bado mashakani kushushwa Daraja!!!!

Wakiwa ugenini Fratton Park, Sunderland walipata bao la utangulizi likifungwa na Kenwyne Jones dakika ya 59 lakini Portsmouth wakasawazisha dakika moja baadae kupitia Mnigeria John Utaka. Dakika ya 68 Beki wa Sunderland Bardsley akajifunga mwenyewe kuwapa uongozi Portsmouth na kosa kubwa alilofanya Anthon Ferdinand wa Sunderland, mdogo wake Rio Ferdinand wa Manchester United, liliwazawadia Portsmouth bao la 3 alilofunga Traore dakika ya 88.
Ingawa Sunderland wako nafasi ya 16 wakiwa na pointi 36 lakini wakifungwa mechi yao ya mwisho watashushwa ikiwa Newcastle na Hull City watashinda mechi zao za mwisho.
Ikiwa Newcastle watashinda na Hull City kutoka droo basi Sunderland [IKIWA HATOFUNGWA ZAIDI YA BAO 5] na Newcastle watapona na badala yake Hull City wataporomoka.
Ili Middlesbrough apone itabidi kwanza ashinde mechi yake na kuomba Hull City na Newcastle wafungwe lakini nani atashushwa kati ya Middlesbrough na Hull City itategemea Middlesbrough kafunga bao ngapi na Hull City kafungwa ngapi.
Hizo, kwa ufupi, ndizo hesabu kali za nani atasalimika kubaki LIGI KUU.
Msimamo kwa Timu za chini zilizo kwenye VITA KUU ya KUJINUSURU KUSHUSHWA DARAJA ni [West Bromwich tayari shashushwa]: [TIMU ZA NAFASI YA 18 HADI 20 HUSHUSHWA]
-Nafasi ya 16: Sunderland pointi 36
-Nafasi ya 17: Hull City pointi 35
-Nafasi ya 18: Newcastle pointi 34
-Nafasi ya 19: Middlesbrough pointi 32
-Nafasi ya 20: West Brom pointi 31
MECHI ZA MOTO ZA MWISHO KWA TIMU HIZI ZA CHINI JUMAPILI IJAYO 24 MEI 2009:
Aston Villa v Newcastle
Hull v Man U
Sunderland v Chelsea
West Ham v Middlesbrough

No comments:

Powered By Blogger