Saturday 23 May 2009

RONALDO MATATANI!!!!

Ronaldo de Lima [32] atafikishwa mbele ya Tume ya Michezo huko Sao Paulo, Brazil baada ya kugundulika alimfinya na kumvuta nywele Beki wa Botafogo aitwae Fahel [pichani].
Ronaldo,ambae aliwahi kuwa Mchezaji Bora Duniani mara 3 na alieiwezesha Brazil kutwaa Kombe la Dunia mwaka 1994 na 2002, hakuonekana na Refa wa pambano hilo la Klabu ya Ronaldo iitwayo Corinthians waliocheza na Botafogo.
Lakini picha za video zilionyesha tukio hilo ambalo lilianza baada ya Beki wa Botafogo Fahel kumvuta jezi Ronaldo na kumchezea rafu na Ronaldo akalipiza kisasi kwa kumfinya na kumvuta nywele Fahel.
Mwendesha Mashtaka wa Tume hiyo ya Michezo Paulo Schmitt amesema ingawa Ronaldo ni supastaa lakini kwenye Tume hiyo kila mtu ni sawa.
Akipatikana na hatia Ronaldo atafungiwa mechi 3.
Lakini kitu cha kushangaza kabisa ni ile hatua ya Mchezaji wa Botafogo Fahel ambae alitendewa makosa hayo kusema yuko tayari kutoa ushahidi ili kumtetea Ronaldo.
Fahel amesema: 'Nadhani alichukizwa wakati ule!! Lakini kinachotokea uwanjani bora kiachwe uwanjani!'
Ronaldo alianza kucheza tena mwezi Machi mwaka huu akichezea Corinthians ya Brazil baada ya kukaa mwaka mmoja nje kwa kuwa majeruhi na tangu wakati huo ameifungia Corinthians mabao 10 hali iliyowafanya mashabiki wengi kumtaka Bosi wa Timu ya Taifa ya Brazil, Dunga, amrudishe tena Kikosini.
Hata hivyo, Dunga juzi aliteua Kikosi cha Brazil bila Ronaldo ambacho kitacheza mechi za mchujo za Kombe la Dunia mwanzoni mwa Juni na baadae kusafiri hadi Afrika Kusini kucheza kwenye Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara [FIFA CONFEDERATION CUP] yanayoanza Juni 14.
Kiungo Boateng wa Hull City ashangazwa na zogo la Kikosi cha Man U watakachocheza nacho kesho!!!
George Boateng, Mchezaji Kiungo wa Hull City ambao kesho wanakutana na Manchester United KC Stadium nyumbani kwa Hull katika mechi ambayo inabidi washinde ili wajinusuru kushushwa Daraja, amesema anashangazwa sana na jinsi mzozo ulivyoibuka wa Kikosi kipi kichezeshwe na Manchester United hapo kesho.
Manchester United, baada ya kuuchukua Ubingwa wa LIGI KUU wiki iliyopita na kukabiliwa na Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE Jumatano ijayo watakapocheza Roma, Italia na Barcelona, wanategemewa kuwapumzisha mastaa wao kwenye mechi ya kesho isiyo na umuhimu wowote kwao.
Boateng anaamini Klabu zenyewe zilizo hatarini kushushwa ndio zijilaumu kwa kuwa katika hali hiyo na sio kutafuta visingizio. Anasema: 'Sir Alex Ferguson msimu wote amekuwa akibadilisha Kikosi chake na wameshinda mechi nyingi. Nilitazama ile Nusu Fainali ya FA CUP na Everton walipopumzisha mastaa wao wengi na wakatolewa kwa penalti na hakuna mtu alielaumu isipokuwa Mashabiki wa Man U waliotaka kwenda Fainali.'
Boateng aliongeza: 'Tunajua Hull City ni Timu ndogo na Nchi nzima inataka Klabu kubwa Newcastle inayoongozwa na Shujaa wa England Alan Shearer ibaki LIGI KUU. Ndio maana hizi kelele za visingizio vya ajabu!!'

No comments:

Powered By Blogger