Sunday 17 May 2009

WEST BROMWICH TIMU YA KWANZA KUSHUSHWA LIGI KUU MSIMU HUU!!

  • Wafungwa 2-0 na Liverpool!!!
  • Almanusura Wachezaji wa Liverpool kutwangana uwanjani!!!!

West Bromwich Albion imeteremshwa Daraja na kurudishwa Daraja la chini liitwalo COCA COLA CHAMPIONSHIP baada ya kupigwa mabao 2-0 na Liverpool.
Mabao ya Liverpool yalifungwa na Steven Gerrard na Dirk Kuyt.
Mechi hii nusura iingie doa kubwa pale Wachezaji wa Liverpool Jamie Carragher na Alvaro Arbeloa walipovaana na kusukumana na ikabidi mwenzao Xabi Alonso aingilie kati kuamulia na pia Refa kuwaonya.
Mchezaji wa West Bromwich asimamishwa kwa tuhuma za kununua Madawa ya Kulevya!!
Mchezaji wa West Bromwich, Roman Bednar kutoka Czech, amesimamishwa na Klabu yake baada ya Gazeti liitwalo 'News of the World' kuandika ripoti kuwa walimfuma akinunua Madawa ya Kulevya.
Chelsea 2 Blackburn 0
Nicolas Anelka alifunga bao moja na kumtengenezea Florent Malouda kufunga bao la pili kayika mechi ya LIGI KUU England iliyochezwa Stamford Bridge ambayo ndiyo ya mwisho kwa Meneja wao Guus Hiidink uwanjani hapo kwani mwishoni mwa msimu anarudi kwenye kazi yake ya kudumu ya kuwa Meneja wa Timu ya Taifa ya Urusi.
STAA WA URENO FIGO KUSTAAFU SOKA!!!
Kiungo Luis Figo ametangaza kustaafu Soka mwishoni mwa msimu huu mara tu baada ya kuisaidia Klabu yake ya Inter Milan kunyakua Ubingwa wa Italia kwa mara ya 4 mfululizo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36 ambae mwaka 2001 ndie alikuwa Mchezaji Bora Duniani alijitengenezea jina lake alipozichezea Barcelona na Real Madrid za Spain.
Figo alihama Barcelona na kwenda Real Madrid mwaka 2000 na mwaka 2002 alichukua Klabu Bingwa Ulaya akiwa na Real.
Mwaka 2005 akahamia Inter Milan ya Italia.
Figo ndie Mchezaji anaeshikilia rekodi ya kuchezea Timu ya Taifa ya Ureno mechi nyingi kwa kucheza mechi 127 na kufunga magoli 32.

No comments:

Powered By Blogger