Wednesday 20 May 2009

Utata Kipa Namba moja England!!!

Golikipa nambari wani wa England, David James, miaka 38, anaedakia Portsmouth amefanyiwa operesheni ya bega na hivyo atazikosa mechi za England za mchujo kuwania nafasi ya kwenda Afrika Kusini mwaka 2010 kwenye Fainali za Kombe la Dunia za mwezi Juni ambapo England watacheza na Kazakhstan na Andorra. Kipa nambari mbili wa England ni Yule Kipa rizevu wa Manchester United, Ben Foster, ambae pia imetangazwa anahitaji operesheni kurekebisha kidole gumba na atazikosa mechi za Klabu yake ile ya mwisho ya LIGI KUU Jumapili na Hull City na Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE na Barcelona. Hivyo Ben Foster nae atazikosa mechi za mwezi ujao za England.
Sasa nafasi iko wazi kwa Kipa wa West Ham Robert Green na hata Kipa wa zamani wa England Paul Robinson wa Blackburn kushika hatamu. Wengine wanaonyatia nafasi hiyo ni Chris Kirkland wa Wigan na Joe Hart wa Manchester City
Wakala wa Mchezaji Antonio Valencia athibitisha Real Madrid wametoa ofa!!!
Mchezaji kutoka Ecuador anaechezea Wigan, Antonio Valencia, inasemekana anatakiwa na Real Madrid na Klabu hiyo ya Spain imeshatoa ofa rasmi ili kumchukua.
Habari hizo zimethibitishwa na Wakala wake, Diego Herrera, na sasa Wigan wanasubiri ofa toka Klabu nyingine ili kumnadi kwa bei poa.
Mwenyekiti Arsenal adai Wenger atabaki Arsenal!!!
Kufuatia utata uliozuka baada ya mgongano kati ya Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, na baadhi ya Wadau wenye hisa Klabuni hapo kwenye mkutano wa hadhara kati ya Wadau na Menejimenti wiki iliyokwisha ambapo Wadau hao walihoji na kumkandya Wenger hasa kwa vile Arsenal haijachukua Kombe lolote tangu mwaka 2005, Mwenyekiti wa Arsenal, Peter Hill-Wood, imebidi aibuke na kutuliza ngoma.
Mzozo huo ulifuatiwa na taarifa zilizogaa kuwa Mgombea Urais wa Real Madrid, Florentino Perez, ambae inasemekana ana uhusiano mzuri na Wenger, ametoa ahadi kuwa akichaguliwa Rais basi Arsene Wenger atatua Santiago Bernabeue.
Habari hizo zikashika mizizi pale Arsene Wenger mwenyewe kuhojiwa na TV Stesheni moja kutoka huko Ufaransa na kukiri kuwa kuhamia Real Madrid kuna mvuto na huko kuna mradi mkubwa.
Mwenyekiti Hill-Wood amewaponda Wadau hao, ambao wengine walidiriki kuhoji hata mbinu za Uchezaji anazotumia Wenger, kwa kuwaambia vitendo hivyo ni makosa na kuhujumu Timu.
Hata hivyo Hill-Wood amethibitisha Wenger ana mkataba na Arsenal hadi 2011 na hategemei kuwa ataondoka.
Beki Cannavaro ahama Real na kurudi Klabu yake ya zamani Juventus!!!
Nahodha wa Timu ya Taifa ya Italia, Fabio Cannavaro, miaka 35, amehama Real Madrid na kurudi kwao Italia kuchezea Juventus kwa mkataba wa mwaka mmoja. Cannavaro alienda Real mwaka 2006 na sasa ataichezea Juventus kuanzia Julai 1, 2009.
Cannavaro, aliyekuwa Mchezaji Bora wa Dunia mwaka 2006, aliihama Klabu ya Juventus mwaka huo huo mara tu baada ya Klabu hiyo kushushwa Daraja baada ya kubainika ilishiriki kwenye njama za kupanga matokeo na Mashabiki wa Juventus walikasirika kwa kuhama kwake. Kurudi kwa Cannavaro Juventus kumetangazwa siku moja tu baada ya kufukuzwa kazi Meneja Claudio Ranieri.
Kikosi cha Man U kitakachocheza na Hull City LIGI KUU Jumapili ijayo chazua mjadala mkali England!!!!
Sir Alex Ferguson ametoa fununu kuwa Kikosi cha Manchester United kitakachocheza mechi ya mwisho ya LIGI KUU England na Hull City Jumapili ijayo, mechi ambayo haina umuhimu wowote kwa Man U kwani kisha uchukua Ubingwa lakini ni ya kufa na kupona kwa Hull City, kitakuwa cha mchanganyiko.
Hull City watawakaribisha Man U KC Stadium huku wakitaka ushindi ili kuepuka kushushwa Daraja na wakati huohuo kuwakandamiza Newcastle na Middlesbrough kuungana na West Bromwich ambao tayari washashushwa Daraja.
Phil Brown, Meneja wa Hull City, amesema: 'Sidhani kama Ferguson atatusaidia!! Ni kweli siku tatu baadae atakuwa na Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE na Barcelona na akili yake yote iko huko lakini ukweli ni kwamba Manchester United wana Kikosi Bora LIGI KUU na wanaweza kuchagua Timu mbili tofauti na kushinda mechi yeyote ile!!! Si rahisi kwetu ni kazi ngumu!!!!'
Baadhi ya watu wameuhusisha uhusiano mzuri wa Sir Alex Ferguson na Phil Brown kuwa huenda ukamsaidia tena Phil Brown na wametaja jinsi Ferguson alivyomsaidia Brown kupata kazi ya Umeneja huko Derby County mwaka 2005.
Alan Shearer, Meneja wa Newcastle, Timu ambayo inagombea kunusurika kushushwa na huenda hatua ya Ferguson ya kuchezesha Kikosi hafifu inaweza kumuathiri, amesema: 'Ningependa Man U wasingekuwa na Fainali ile siku tatu baadae!! Lakini siwezi kumwambia chochote Ferguson!! Lakini hali kama hii ishatokeo hapo nyuma na Ferguson amekuwa mkweli kwani alitazama mazingara ya msimamo wa ligi na kuchagua Kikosi kilichomridhisha kila mtu!!! Huo ndio ubora wa Ferguson!!!'
Ferguson mwenyewe amesema: 'Hiki ni Kikosi bora nilichonacho!! Jumamosi na Arsenal ningeweza kuteua Timu mbili tofauti na Jumapili ijayo ntateua Timu inayostahili. Nina Kikosi cha Wachezaji 28 au 29 wakiwemo chipukizi Macheda, Webeck, Possebon na mapacha Da Silva. Najua ni vijana lakini ni Wachezaji wazuri sana!!!

No comments:

Powered By Blogger