Monday 18 May 2009

KITIMTIM KWA SUNDERLAND LEO: Portsmouth v Sunderland

  • Sunderland watajinusuru kushuka Daraja leo??

Portsmouth na Sunderland leo saa 4 usiku, saa za bongo, wanavaana Uwanjani Fratton Park nyumbani kwa Portsmouth kwenye mechi ya LIGI KUU England ambayo haina umuhimu kwa Portsmouth kwani matokeo ya mechi za juzi na jana zimewaepusha kushuka Daraja lakini kwa Sunderland ni mechi ya kufa na kupona.

Sunderland, ambao wako pointi mbili juu ya zile Timu tatu za mwisho zilizo eneo la kuporomoka Daraja, wakishinda leo basi watajihakikishia kubaki LIGI KUU lakini wakifungwa au kutoka suluhu itabidi wasubiri hadi Jumapili ijayo kujua usalama wao wakati Timu zote za LIGI KUU zitacheza mechi za funga dimba za LIGI KUU msimu huu wa mwaka 2008/9.

Timu tatu za mwisho na ambazo ziko kwenye eneo la kuteremshwa Daraja ni Newcastle, Middlesbrough na ile ya mkiani, West Bromwich Albion, ambayo jana iliaga rasmi LIGI KUU baada ya kupigwa 2-0 na Liverpool.

No comments:

Powered By Blogger