Monday 18 May 2009

VIDIC ASHINDA TUZO MBILI KLABUNI KWAKE MAN U!!

Beki mahiri wa Mabingwa Manchester United, Nemanja Vidic, ametunukiwa Tuzo mbili Klabuni kwake Manchester United baada ya kushinda kura na kuchaguliwa Mchezaji Bora wa Msimu anaechaguliwa na Wachezaji Wenzake na nyingine Mchezaji Bora wa Msimu anaechaguliwa na Washabiki.


Vidic, miaka 27, kutoka Nchi ya Serbia aliehamia Manchester United kutoka Spartak Moscow miaka mitatu iliyopita akishirikana na Beki mwenzake Rio Ferdinand, walipewa pongezi za dhati kwa kuweka ngome imara katika Chakula cha Usiku kilichotayarishwa ili kutoa Tuzo hizo.


Cristiano Ronaldo, Mshindi wa Tuzo hizo Msimu uliopita, safari hii alishinda Tuzo ya Goli la Mwaka kwa goli alilofunga kwenye mechi ya Man U na FC Porto ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE alipoachia kigongo cha mita kama 40.


RANIERI AFUKUZWA JUVENTUS!!!


Claudio Ranieri, aliewahi kuwa Meneja wa Chelsea, leo ametimuliwa kazi na Bodi ya Juventus baada ya kutoridhika na uongozi wake.


Ranieri alipewa kazi ya Umeneja Juventus Juni 2007 lakini hakuna mafanikio yeyote yaliyopatikana na huu ni msimu wa 7 sasa Juventus haijatwaa Ubingwa wa Italy na hata msimu huu, huku kukiwa kumaebaki mechi 2 ligi kwisha, wako nafasi ya 3 wakiwa mbele ya Fiorentina kwa pointi moja tu na wakipitwa watapoteza nafasi ya kuingia moja kwa moja ya Makundi ya kugombea UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu ujao.


No comments:

Powered By Blogger