Thursday 9 July 2009

Copa Libertadores Fainali: Estudiantes 0 Cruzeiro 0!
Katika mechi ya kwanza ya Fainali ya Kombe la Klabu Bingwa za Nchi za Marekani ya Kusini, ambayo ni Fainali ya 50 ya Mashindano hayo maarufu kwa jina la COPA LIBERTADORES, jana Timu za Nchi Mahasimu Kisoka Argentina na Brazil , Klabu ya Estudiantes ya Argentina na Cruzeiro ya Brazil zilitoka suluhu 0-0.
Fainali hii inachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na mechi ya jana ilichezwa Argentina na marudiano yatafanyika Brazil wiki ijayo tarehe 15 Julai.
‘Uhamisho wa Kiwehu’ wamtia uchizi Benitez!
Meneja wa Liverpool Rafael Benitez ametoboa kuwa Klabu yake imeshindwa kushindana katika Soko la kununua Wachezaji kwa vile bei ni za ‘kiwehu!’.
Hivi juzi tu Liverpool ilitoa Pauni Milioni 17 kumnunua Beki wa Kulia wa Portsmouth Glen Johnson lakini ikamkosa Mchezaji waliekuwa wakimwania kwa muda mrefu Gareth Barry aliechukuliwa na Manchester City.
Vilevile, inabidi Benitez apigane ili kunusuru Xabi Alonso na Javier Mascherano wasimponyoke kwani kuna imani kubwa wanatakiwa na Vigogo wa Spain Real Madrid.
Benitez amegomba: ‘Soko ni la kiwehu! Sasa ni pesa, pesa, pesa tu sasa!’
Hata hivyo ameonya Timu zinazotumia pesa nyingi kununua Wachezaji kwamba kitabu cha hundi hakihakikishi Timu inapata mafanikio.
Rais wa Barca aikandya Real!!!
Rais wa Barcelona, Joan Laporta, amewaponda Mahasimu wao wakubwa huko Spain, Real Madrid kwa kutumia pesa nyingi sana kununua Wachezaji.
Real Madrid imewanunua Ronaldo, Kaka, Albiol na Benzema yuko njiani na jumla ya pesa zilizotumika kuwapata Wachezaji hao wanne ni zaidi ya Euro Milioni 200.
Laporta amekaririwa akisema: ‘Sisi Tunatengeneza Wachezaji wanaoshinda Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani, sisi hatununui Mchezaji Bora Duniani! Real wamejikita sokni na la kulipotosha Soko la Wachezaji duniani! Sisi hatuko hivyo!’
Wakati huohuo, Laporta amethibitisha kuwa Mchezaji wa Cameroun, Samuel Eto,o, ambae anawaniwa na Manchester City, amepewa nyongeza ya mkataba wa miaka miwili lakini mpaka sasa hajapatikana kuthibitisha.
Laporta amesema: ‘Nimempigia Eto’o mara kadhaa lakini simu yake ya mkononi haipokelewi. Sijui kama kabadilisha namba au kaipoteza!’
Boro yawatwanga faini Wachezaji Mido na Alves!!!
Meneja wa Middlesbrough Timu iliyoporomoka kutoka Ligi Kuu England msimu uliokwisha, Gareth Southgate, amethibitisha Wachezaji wao Mido kutoka Misri na Alfonso Alves wa Brazil wamechukuliwa hatua za kinidhamu na Klabu hiyo ikiwa pamoja na kukatwa mishahara ya wiki mbili kwa kuchelewa kuripoti kwenye mazoezi ya kujitayarisha na mwanzo wa msimu mpya wa Daraja la chini liitwalo Coca Cola Championship unaoanza mwezi Agosti.
Wachezaji hao wawili walitakiwa waanze mazoezi Jumatatu lakini hawakuonekana na ingawa Alves amesharipoti Mido bado yuko mitini.

No comments:

Powered By Blogger