Thursday 9 July 2009

Ziara ya Man United kabla msimu kuanza!!!
Mabingwa Manchester United wameanza mazoezi kwenye Kituo chao cha mazoezi huko Carrington, Manchester wakijitayarisha kwa ziara ya Asia watakayoianza Juali 16 kwa kuruka hadi Kuala Lumpur, Malaysia ambako watacheza mechi ya kwanza Uwanja wa Bukit Jalil Julai 18 na Kombaini ya Malaysia.
Baada ya hapo watakwenda Jakarta, Indonesia kucheza na Timu ya Mchanganyiko wa Wachezaji wa Ligi Kuu ya Indonesia Julai 20.
Julai 24 watakuwa Mji Mkuu wa Korea ya Kusini, Seoul, kucheza na Klabu ya FC Seoul kwenye Uwanja wa Kombe la Dunia Seoul.
Kisha, Man U wataruka hadi Uchina kucheza na Hangzhou Greentown Julai 26 Uwanjani Huanglong Sports Center.
Kutoka China, Man U wataenda moja kwa moja hadi Ujerumani kushiriki kwenye Kombe la Audi na tarehe 29 Julai watakwaana na Vigogo wa Argentina Boca Juniors kwenye Uwanja wa Klabu ya Bayern Munich uitwao Allianz Arena.
Siku ya pili, Man U watacheza na na Bayern Munich au AC Milan ikiwa ama ni mechi ya Fainali ya Kombe hilo la Audi au ya kutafuta Mshindi wa tatu ikitegemea matokeo kati ya mechi za Man U na Boca Juniors na ile ya Wenyeji Bayern Munich na AC Milan.
Manchester United watakuwa nyumbani Old Trafford Agosti 5 kucheza mechi ya kirafiki na Klabu ya Spain, Valencia.
Jumapili, Agosti 9, ndani ya Uwanja wa Wembley, ile mechi ya ‘Fungua Pazia la Msimu Mpya’ ijulikanayo kama Ngao ya Hisani itachezwa, na Manchester United, wakiwa Mabingwa wa Ligi Kuu, watapambana na Chelsea, Mabingwa wa Kombe la FA.
Wiki inayofuata, Jumapili Agosti 16, siku moja baada ya LIGI KUU England kuanza rasmi, Manchester United wataanza rasmi kutetea Ubingwa wao katika Ligi hiyo kwa kuikaribisha Timu iliyopanda Daraja, Birmingham, Uwanjani kwake Old Trafford.

No comments:

Powered By Blogger