Sunday 5 July 2009

Redknapp akiri Man City imempiku kuwachukua Barry na Santa Cruz!
Bosi wa Tottenham, Harry Redknapp, amekiri kuwa Manchester City waliwashinda ubavu kwa kuwa na uwezo mkubwa na ndio maana wakaweza kuwachukua Wachezaji Gareth Barry kutoka Aston Villa na Roque Santa Cruz kutoka Blackburn Rovers ambao wao pia walikuwa wanawawania.
Redknapp amesema uwezo wa Man City kulipa ada kubwa na kuwalipa Wachezaji mishahara minono ndio unaowawezesha kuchukua Wachezaji kwa bei mbaya.
Hata hivyo Redknapp amesema Tottenham hawana papara ya kukurupuka kununua Wachezaji na hata kama hawakupata mtu msimu huu ana imani na Kikosi kilichopo.
Beckenbauer aisapoti England kuwa Mwenyeji Fainali za Kombe la Dunia
Mchezaji wa zamani wa Ujerumani na Mshindi wa Kombe la Dunia Franz Beckenbauer anaamini bila wasiwasi kuwa England ina uwezo wa kuendesha Fainali za Kombe la Dunia kwa sababu wana Viwanja vingi vya kisasa na pia Washabiki wengi sana.
Franz Beckenbauer, Nahodha wa zamani wa Ujerumani, yumo kwenye Kamati ya FIFA itayoamua nani Mwenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 na 2022.
Beckenbauer amekaririwa akisema: ‘Hata wakiambiwa wawe Wenyeji kesho, England wanao uwezo kwa sababu wana miundo mbinu ya kisasa, Washabiki, Viwanja na kila kitu kinachotakiwa kwa Fainali hizo.’
England ni miongoni mwa Nchi 9 zinzogombea Uenyeji wa Fainali za 2018 na wapo katika Nchi 11 zinazogombea zile za 2022.
FIFA itaamua Desemba nani watakuwa Wenyeji.
Tevez: ‘Mimi sio msaliti!’
Carlos Tevez amewakikishia Mashabiki wa Manchester United kuwa akijiunga na Wapinzani wa Manchester United, Manchester City, atakuwa haisaliti Klabu hiyo aliyochezea misimu miwili kwa kuwa sababu ya kuondoka yeye ni Man U na si yeye.
Hata hivyo, Manchester United walikuwa tayari kulipa pesa za kumnunua Tevez toka Kampuni inayommliki na pia walishampa ofa ya mkataba wa miaka mitano na mshahara mkubwa tu ambao ungemfanya Tevez awe mmoja wa Wachezaji wa Man U wanaolipwa donge nono sana, lakini Tevez aligoma kwa madai kuwa msimu uliokwisha alidharauliwa kwa kutopangwa mara kwa mara.
Mkataba wa Tevez na Manchester United ulimalizika Juni 30.

No comments:

Powered By Blogger