Tuesday 7 July 2009

Kipa Ben Foster asaini mkataba mpya Man U!!
Kipa Ben Foster, miaka 26, amesaini mktaba mpya wa miaka minne na Klabu yake Manchester United ambao utamuweka Old Trafford hadi 2013.
Foster, ambae pia anachezea Timu ya Taifa ya England, ndie anaeonekana ni mrithi wa Edwin van der Sar anaestaafu mwakani na alichukuliwa na Man u kutoka Stoke City mwaka 2005.
Kupanda chati kwa Foster kumekuwa kwa hati hati kwani amekuwa akikumbwa na majeruhi ya mara kwa mara ikiwa na pamoja kuukosa mwisho wa msimu uliopita baada ya kuumia kidole gumba cha mkono na kufanyiwa operesheni
Kipa Paddy Kenny wa Sheffield United agundulika katumia madawa yaliyopigwa marufuku!
Kipa Paddy Kenny wa Sheffield United amesimamishwa na Klabu yake Sheffield United baada ya kugundulika amefeli vipimo vya uchunguzi na kuonekana ametumia madawa ambayo hayaruhusiwi.
Ugunduzi huo uliotokea baada ya kupimwa kwenye mechi ya mchujo wa kupanda Daraja mwezi Mei ambayo Sheffield United walicheza na Preston na kuonekana ana chembe chembe za dawa ‘Ephedrine’ ambayo ni marufuku kwa Wanamichezo kwa sababu huongeza nguvu.

Dawa hiyo hutumika kutibu mafua na kutuliza pumu.
Kipa Kenny sasa atachunguzwa na FA na huenda akatumikia kifungo cha miaka miwili.
Bosi wa Chelsea adai Terry hauzwi!!
Bosi wa Chelsea, Peter Kenyon, ametangaza kuwa Nahodha wao John Terry hauzwi licha ya kufukuziwa kwa karibu sana na Manchester City.
Kenyon anaungana na Meneja mpya, Carlo Ancelotti,aliedai jana kuwa Nahodha huyo atabaki Stamford Bridge.
Kenyon ametamka: ‘Ana mkataba wa miaka mitatu. Mwenyewe amesema hataki kuondoka na sisi hatutaki aondoke. Mwisho wa hadithi!’
Winga Chipukizi wa Ufaransa apimwa afya Man U!!!!
Gabriel Obertan, miaka 20, anaechezea Timu ya Taifa ya Vijana wa Ufaransa wa chini ya miaka 21 na Klabu ya Bordeaux, leo amepimwa afya yake Manchester United ili anunuliwe.
Obertan, aliekuwa pia akitakiwa na Klabu za AC Milan, Inter Milan na Arsenal, ameichagua Manchester United na Meneja wake huko Bordeaux, Laurent Blanc, aliewahi kuichezea Man U, ameonyeshwa kushtushwa kwa Man U kumtaka Mchezaji huyo ingawa amesema ni nafasi bora kwa Winga huyo.
Mrusi Yuri Zhirkov njiani kwenda Chelsea!!
Mchezaji wa Kiungo wa Timu ya Urusi na Klabu ya CSKA Moscow, Yuri Zhirkov, amefanyiwa upimaji wa afya Klabuni Chelsea ili wamsajili.
Zhirkov, miaka 25, anathaminiwa kuwa ada yake itakuwa kwenye Pauni Milioni 18.
Mbrazil Jo kubaki Everton kwa mkopo!!
Straika wa Manchester City kutoka Brazil, Jo, ataendelea kubaki Everton kwa mkopo wa mwaka mmoja zaidi baada ya Klabu hizo kufikia makubaliano.
Msimu uliokwisha Jo alichezea Everton kwa mkopo na kucheza mechi 12 na kufunga bao 5.
Jo alinunuliwa na Manchester City kutoka CSKA Moscow lakini hakupata mafanikio Klabuni hapo.
Kwa sasa, Man City wanawawinda Samuel Eto’o kutoka Barcelona na Carlos Tevez ambae hana Klabu.
Ronaldo atambulishwa mbele ya Mashabiki 80,000 Uwanjani Bernabeau!!!
Cristiano Ronaldo ameanuliwa rasmi kama Mchezaji wa Real Madrid mbele ya Mashabiki 80,000 waliofurika Uwanjani Santiago Bernabeau.
Ronaldo amehamia Real kwa ada ambayo ni rekodi ya dunia ya Pauni Milioni 80.
Lakini mwishoni mwa sherehe hizo Washabiki hao walivamia Uwanja na ilibidi Polisi wamkimbize Ronaldo ili kumuokoa.

1 comment:

Anonymous said...

walivamia uwanja kwa lengo gani furaha ya kumpata au chuki kwakuwa kanunuliwa kwa dau kubwa?tufafanulie

Powered By Blogger