Wednesday 8 July 2009

PELE ABASHIRI NCHI YA AFRIKA INAWEZA KUTINGA FAINALI KOMBE LA DUNIA AFRIKA KUSINI 2010!!
Edson Arantes Do Nascimento, maarufu Duniani kote kama Pele [pichani akimkabidhi Ronaldo Tuzo ya Mchezaji Bora Duniani], ametabiri mojawapo ya Nchi za Afrika inaweza ikaingia Fainali ya Kombe la Dunia mashindano hayo yakichezwa mwakani huko Afrika Kusini.
Pele alitoa utabiri huo alipokuwa Abuja, Nigeria akiisaidia Nchi yake Brazil ili ipate Uenyeji wa Mashindano ya Olimpiki ya mwaka 2016 kwenye Baraza Kuu la Vyama vya Olimpiki vya Afrika.
Pele alisema kauli yake inaungwa mkono na uwezo walioonyesha Afrika Kusini kutinga Nusu Fainali ya Kombe la Mabara wiki mbili zilizoisha na pia Marekani kucheza Fainali ya Kombe hilo.
Pele alisema: ‘Kwa sasa hamna Timu ndogo au Nchi ndogo.’
Alipoulizwa kwa sasa anashughulika na nini Pele alijibu: ‘Nipo na FIFA na pia na watoto shuleni. Nipo kwenye Kamati mojawapo ya FIFA. Miaka 6 iliyokwisha nilikuwa Waziri wa Michezo Brazil na nilipata Marafiki wengi duniani.’

No comments:

Powered By Blogger