Monday 6 July 2009

Glenn Hoddle: Owen ni bora kupita Tevez kwa Man U!
Kocha wa England mwaka 1998 Glenn Hoddle aliempa Jezi Michael Owen kuchezea England kwa mara ya kwanza na kuifunga Argentina mwaka huo huo kwa goli la ajabu sana kwenye Kombe la Dunia, wakati Owen ni Kinda tu, amepasua na kusema Sir Alex Ferguson amefanya uamuzi busara na wa akili kubwa kumchota Michael Owen kucheza Old Trafford.
Hoddle ametamka: ‘Ni biashara nzuri Ferguson kafanya! Nina uhakika kama Michael atabaki fiti na atacheza mechi 30 au zaidi atafanya vizuri sana kupita Tevez! Jinsi Man U wanavyocheza Owen atakuwa bora tu!’
Glenn Hoddle akaongeza: ‘Man U wanamiliki na kutawala mpira, wanatengeneza nafasi nyingi za kufunga na hio ni bora kwa Owen ambae ni mmaliziaji hatari! Owen atang’ara Man U!’
Hoddle akawakumbusha watu kuhusu Eric Cantona, Teddy Sherigham na Henrik Larsson ambao wote maisha yao Kisoka yalielekea ukingoni lakini Ferguson akawavuta Man U na wakawika na pia kuiletea mafanikio Man U.

No comments:

Powered By Blogger