Wednesday 8 July 2009

Copa Libertadores leo Fainali: Estudiantes v Cruzeiro!
Leo ni Fainali ya Kombe la Klabu Bingwa za Nchi za Marekani ya Kusini na ni Fainali ya 50 ya Mashindano hayo maarufu kwa jina la COPA LIBERTADORES na leo inazikutanisha Timu za Nchi Mahasimu Kisoka Argentina na Brazil wakati Argentina watawakilishwa na Klabu ya Estudiantes na Brazil ni Cruzeiro.
Fainali hii inachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na mechi ya leo itachezwa Argentina na marudiano yatafanyika Brazil wiki ijayo tarehe 15 Julai.
Hii ni mara ya pili kwa Klabu hizi mbili kukutana kwenye Kombe hili msimu huu kwani walikuwa Kundi moja katika mechi za awali ambapo mechi ya kwanza Cruzeiro iliifunga Estudiantes 3-0 huko Brazil na marudiano huko Argentina, Estudiantes ilishinda 4-0.
Cruzeiro inae Mchezaji, Kleber, ambae wengi watamkumbuka kwani alicheza hivi juzi Kombe la Mabara huko Afrika Kusini na kuisaidia Brazil kutwaa Kombe hilo.
Nao, Estudiantes wanae Mkongwe Juan Sebastian Veron ambae aliwahi kuichezea Manchester United.
Mechi hii itanza saa 7 na nusu usiku saa za kibongo.
Zokora ahama Spurs kwenda Sevilla
Sevilla wamemsaini Mchezaji wa Tottenham anaetoka Ivory Coast Kiungo Didier Zokora kwa ada ambayo haikutajwa.
Zokora, 28, ameichezea Spurs mechi 134 na sasa amesaini mkataba wa miaka minne na Sevilla ya Spain. Sevilla inategemea kumtambulisha Zokora mbele ya Washabiki wao leo jioni.

No comments:

Powered By Blogger