Saturday 11 July 2009

Campbell wa Man U aenda Sunderland!
Kijana wa Manchester United Frazier Campbell, miaka 21, ambae alikuwa akicheza kwa mkopo Tottenham msimu uliokwisha ikiwa ni mapatano yaliyomfanya Dimitar Berbatov kusaini Man U, hatimaye amenunuliwa na Steve Bruce, Meneja mpya wa Sunderland, na kufanya Campbell awe Mchezaji wake wa kwanza Bruce kumnunua.
Campbell alitegemewa sana kwenda Hull City Timu ambayo aliichezea kwa mkopo msimu wa 2007/8 na kuisaidia kupanda kuingia LIGI KUU lakini ameichagua Sunderland ya Steve Bruce aliewahi kuichezea Man U.

No comments:

Powered By Blogger