Sunday 5 July 2009

Sunderland wanamfukuzia Mlinzi Da Silva toka Paraguay!!
Meneja wa Sunderland, Steve Bruce, yuko mbioni kumsaini Mlinzi wa Klabu ya Deportivo Toluca, Paulo Da Silva kutoka Paraguay ili awe Mchezaji wake wa kwanza kumsajili.
Steve Bruce amehamia Sunderland kutoka Wigan mara tu baada ya Ligi Kuu kumalizika katikati ya mwezi Mei.
Paulo Da Silva, umri miaka 29, ni Mchezaji huru baada ya mkataba wake kumalizika na Klabu yake Deportivo Toluca iliyothibitisha kuwa baada ya Sunderland kuonyesha nia ya kumchukua Mchezaji huyo mwenyewe aligoma kuongeza mkataba.
Inasadikiwa Da Silva atasafiri kwenda England wiki ijayo ili kukamilisha taratibu za uhamisho.
Mkongwe Mark Viduka atathmini ofa toka Klabu mbili za Ligi Kuu
Mchezaji wa zamani wa Newcastle, Veterani Mark Viduka, ambae mkataba wake na Klabu hiyo ulimalizika wiki iliyokwisha anatafakari ofa toka Klabu mbili za Ligi Kuu ambazo hazikutajwa ingawa mojawapo inaaminika ni Fulham.
Viduka, mwenye umri wa miaka 33, anapenda abaki England ili ajiongezee matumaini ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwakani akiwa na Nchi yake Australia ambayo tayari imefuzu kuingia Fainali hizo.
Wakala wa Mark Viduka, Steve Kutner, amekiri kuwa zipo Klabu mbili kubwa za Ligi Kuu zenye nia ya kumchukua Viduka ingawa hakuzitaja.

No comments:

Powered By Blogger