Saturday 4 July 2009

Ili kumchota Melo toka Fiorentina, Arsenal watoe ‘vijisenti’ pamoja na Eboue!!
Wakitaka kumchukua Kiungo Felipe Melo alieng’ara sana kwenye mechi za hivi karibuni za Timu ya Taifa ya Brazil za mchujo za Kombe la Dunia la Kundi la Nchi za Marekani ya Kusini pamoja na Kombe la Mabara huko Afrika Kusini, Arsenal wameambiwa na Klabu ya Melo Fiorentina ya Serie A, Italia, ni lazima watoe dau nono na pia Emmanuel Eboue achukuliwe na Fiorentina.
Mbrazil, Felipe Melo, umri miaka 25, ameongeza mkataba kwa mwaka mmoja zaidi hapo Juni 30 ambao pia una kipengele cha Klabu yake Fiorentina kulipwa Pauni Milioni 21 ili ahame kabla mkataba kumalizika.
Melo alinunuliwa na Fiorentina kwa Pauni Milioni 7 kutoka Klabu ya Spain Almeria mwaka jana na baada ya kushirikiana na Kiungo wa zamani wa Arsenal, Gilbero Silva, kwenye Timu ya Brazil katika mechi za hivi karibuni na kung’ara, chati yake imepanda.
Melo, kwa sasa, ana mkataba na Fiorentina hadi mwaka 2013 na tangu acheze huko Italia amepata sifa ya kuwa Kiungo mpiga makwanja vizuri kitu kilichomsababisha apate Kadi za Njano 17 na Kadi Nyekundu 3 kwa msimu mmoja tu aliocheza Serie A huko Italia. Eboue, Mchezaji kutoka Ivory Coast, msimu uliokwisha alipata msukosuko mkubwa huko Uwanjani Emirates hasa baada ya kuzomewa Desemba 2008 hapo Emirates kwenye mechi dhidi ya Wigan baada ya kuingizwa kutoka benchi na kucheza Soka bovu.

No comments:

Powered By Blogger