Sunday 28 June 2009

KOMBE LA MABARA: Mchezaji gani leo kunyakua MPIRA wa DHAHABU wa ADIDAS?
FIFA, kupitia Kundi lake la Kitaalam, limeteua wachezaji 10 walioshiriki Kombe la Mabara huko Afrika Kusini wakitoka Timu za USA, Brazil, Spain na Afrika Kusini, ili kugombea Tuzo ya Adidas ya Mpira wa Dhahabu ili kuashiria ndie Mchezaji Bora wa Mashindano hayo.
Watakaowapigia kura Wachezaji hao 10 ni Waandishi wa Habari walioruhusiwa kuripoti Mashindano hayo huko Afrika Kusini na kila Mwandishi atatakiwa ateua Wachezaji wake Bora wa tatu na kuwapa wa kwanza pointi 5, wa pili pointi 3 na wa tatu pointi moja.
Mara tu baada ya mechi ya Fainali kumalizika, FIFA itajumlisha pointi hizo kutoka kwa hao Waandishi wa Habari na kumtangaza nani alienyakua Tuzo ya Mpira wa Dhahabu wa Adidas, wa pili atapewa Mpira wa Fedha na yule wa 3 atapata Mpira wa Shaba.
Wachezaji 10 watakaopigiwa kura ni:
DEMPSEY, Clint (USA)
DONOVAN, Landon (USA)
KAKA (Brazil)
LUIS FABIANO (Brazil)
PARKER, Bernard (South Africa)
PIENAAR, Steven (South Africa)
ROBINHO (Brazi)
TORRES, Fernando (Spain)
VILLA, David (Spain)
XAVI (Spain)
Washindi waliopita wa Tuzo ya Mpira wa Dhahabu wa Adidas wa Kombe la Mabara la FIFA na mwaka waliochukua ni:
1997 - Denilson (Brazil)
1999 - Ronaldinho (Brazil)
2001 - Robert Pires (Ufaransa)
2003 - Thierry Henry (Ufaransa)
2005 - Adriano (Brazil)

No comments:

Powered By Blogger