Saturday 4 July 2009

Owen ashangazwa kuchukuliwa na Man U!!
Michael Owen amekiri kuwa hakutegemea kama Manchester United ingeweza kumtaka lakini anaamini kuwa anajiunga na Timu ya washindi.
Akiwa na umri wa miaka 29, Owen mwenyewe anajua siku zake bora zimepita lakini bado ana imani kuwa anaweza kuchangia ili Manchester United ipate mafanikio msimu ujao.
Owen amesema: ‘Ukizungumzia Manchester United siku zote unajua ni Washindi, Vikombe, Uwanja mkubwa na Mashabiki Mamilioni! Kuna Wachezaji bora hapa! Ndio maana wamepata mafanikio makubwa sana! Nadhani sitopata usingizi nikifikiria kuchukuliwa na Manchester United!’
Owen amekiri: ‘Katika miaka michache iliyopita niligundua Sir Alex alikuwa amenikubali kuwa nnao uwezo wa kucheza! Siku zote nilikuwa nikiomba aniombe nichezee Man U! Mie sio mjinga, najua kuna watu wanahisi sina tena uwezo lakini tungoje msimu uanze na nitazungumza nikiwa uwanjani!’
Possebon wa Man U aenda Ureno SC Braga kwa mkopo!!
Mchezaji Rodrigo Possebon, umri miaka 20, aliezaliwa Brazil, amechukuliwa kwa mkopo na Klabu ya Ureno SC Braga na ataisaidia Klabu hiyo itakayocheza Ligi mpya huko Ulaya inayoitwa UEFA Europa League msimu ujao.
Possebon, ambae ni Kiungo na ameshaichezea Timu ya Taifa ya Italia ya Vijana chini ya miaka 20, msimu uliokwisha alicheza Manchester United mechi chache na muda mwingi alikuwa akicheza Timu ya Akiba.
Wakati huohuo, Chipukizi wa miaka 16 kutoka Klabu ya Empoli ya Italia anaeitwa Alberto Massacci anaecheza kama Beki wa pembeni ametamka yuko njiani kujiunga na Manchester United baada ya kufanya mazungumzo na Sir Alex Ferguson.
Habari hizi hazijathibishwa na Manchester United na bila shaka zitazua zogo kubwa huko Italia kwani Chipukizi huyo anasemekana ni Mchezaji anaeonyesha matumaini makubwa ya kuwa bora huko usoni na Klabu za Italia zinashindwa kuwazuia kuondoka kwa vile sheria zinawabana kuwasaini Wachezaji chini ya miaka 18 na hali kama hii ni sawa kama ile ya Chipukizi nyota wa Manchester United, Federico Macheda, aliechukuliwa na Man U.
Ronaldo: ‘Ferguson yuko moyoni mwangu!’
Cristiano Ronaldo amekiri kuwa Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, yuko moyoni mwake na siku zote atamuenzi.
Ronaldo ametoa matamshi hayo huku Real Madrid wakijitayarisha kumtambulisha kama Mchezaji wao hapo Jumatatu kufuatia uhamisho ulioweka rekodi ya ada kubwa kupita zote ya Puni Milioni 80 kutoka Klabu ya Manchester United.
Sir Alex Ferguson alimnunua Ronaldo kutoka Klabu ya Ureno ya Sporting Lisbon kwa Pauni Milioni 12.2 mwaka 2003 na amemwezesha kuwa Mchezaji Bora Duniani.
Ronaldo ametamka: ‘Yeye ni Baba yangu kwenye michezo! Ni mtu muhimu sana kwenye maisha yangu! Inabidi nimshukuru kwa yote aliyonifundisha! Yeye ndio msingi wangu! Siku zote nitampenda na atakuwa moyoni mwangu! Vilevile nawashkuru Mkurugenzi Mkuu David Gill na Wakurugenzi wote!
Ronaldo pia amesema hivi karibuni atasafiri hadi Manchester ili kwenda kumshkuru Ferguson na pia alitoa shukrani zake za dhati kwa Mashabiki wa Man U kwa kusema: ‘Ni nyumbani kwangu! Nimecheza misimu 6 na siku zote walinipenda na kuniimba! Ni mashabiki spesho!’

No comments:

Powered By Blogger