Friday 3 July 2009

Michael Owen huenda akajiunga na Man U!!!
Mshambuliaji Michael Owen leo alikwenda Uwanja wa Carrington ambako ndipo kambi ya mazoezi ya Klabu ya Manchester United kupimwa afya yake ikiwa ni hatua thabiti ya kumfanya ajiunge na Mabingwa hao.
Owen ameondoka Newcastle baada ya mkataba wake kumalizika na yeye mwenyewe kugoma kuuongeza kwa Klabu hiyo iliyoporomoka Daraja.
Owen, mwenye umri wa miaka 29, amekuwa pia akiwindwa na Klabu za Hull City na Stoke City lakini kwa sasa, akifaulu vipimo vya afya , atakuwa Mchezaji wa Manchester United.
Sir Alex Ferguson , baada ya kuondokewa na Ronaldo na Tevez, yuko mbioni kuimarisha Kikosi chake na tayari ameshamsaini Winga Luis Antonio Valencia kutoka Wigan na nia ya kumchukua Owen bila shaka imekuja baada ya kuvutiwa na uzoefu wa Owen katika ufungaji ingawa hivi miaka ya karibuni amekuwa akiandamwa na majeruhi ya mara kwa mara.
Bila shaka kujiunga kwa Owen Manchester United kutapokewa kwa maudhi makubwa na Washabiki wa Liverpool kwani Owen ndiko alikoanza kuchezea Soka tangu utoto na akadumu kwa miaka 8 na kisha kuhamia Real Madrid mwaka 2004 na huko alikaa mwaka mmoja na kununuliwa na Newcastle kwa mkataba wa miaka minne.
Owen pia ameichezea England mara 89.
Chelsea yagoma Nahodha wao Terry kwenda Man City!!
Klabu ya Chelsea, kwa mara ya pili sasa, imeikataa ofa ya Manchester City ya kutaka kumnunua Nahodha wao John Terry na habari hizi zimethibitishwa na Maafisa wa Stamford Bridge.
Msimu uliokwisha, Man City pia walitoa ofa ya kumnunua Terry lakini wakagomewa.
Wenger ana uhakika Adebayor haondoki!
Rais Laporta wa Barca adai Fabregas anaitaka Barcelona!!!
Bosi wa Arsenal, Arsene Wenger, amesema ana uhakika Mshambuliaji wake Emmanuel Adebayor haondoki kwenda kujiunga na AC Milan lakini akitaka mwenyewe kuondoka hawezi kumzuia.
Kwa muda mrefu sasa, Mshambuliaji huyo kutoka Togo amehusishwa na Klabu hiyo ya San Siro na mwenyewe ameelezwa kuwa anapenda kwenda huko kwa sababu Arsenal haijapata mafanikio yeyote tangu 2005 walipochukua FA Cup.
Wenger ameongeza pia kuwa endapo Adebayor ataondoka basi angependa kumchukua mshambuliaji wa Bordeaux ya Ufaransa Marouane Chamakh kama mbadala wake na amedokeza kuwa Mchezaji huyo kutoka Morocco amekubali kuja Arsenal.
Wakati huohuo, Joan Laporta wa Brcelona ya Spain, amedai kuwa Kiungo na Nahodha wa Arsenal, Cesc Fabregas, ana nia ya kujiunga na Mabingwa hao wa Ulaya.
Cesc Fabregas, umri miaka 22, alikuwa Mchezaji wa Timu ya Vijana huko Barcelona na aliihama Klabu hiyo miaka 6 iliyopita na kujiunga na Arsenal na sasa, kufuatana na Lporta, anataka kurudi kwao Spain.
Lakini mpaka sasa hamna dalili yeyote kutoka kwa Fabregas mwenyewe kuwa ana nia hiyo kwani ni wiki iliyokwisha tu alitamka waziwazi nia yake kubakia Emirates Stadium.
Bayern Munich bado inamwinda Bosingwa!
Klabu Kongwe ya Ujerumani, Bayern Munich, bado ina nia ya kumnunua Mlinzi wa Ureno Jose Bosingwa kutoka Chelsea na nia hiyo imethibitishwa na Mwenyekiti wa Bayern, Karl-Heinz Rummenigge.
Rummenigge amesema Klabu yao ipo kwenye majadiliano kamambe na Chelsea na wana uhakika watamnasa Beki huyo ambae inategemewa ataziba pengo la Willy Sagnol aliestaafu.

1 comment:

Anonymous said...

sio siri mdau huyo Adebayor mimi simzimikii kabisa kuwa hapo Arsenal ametukosesha ubingwa kwa ubishoo wake..hivi huyu Arsen Wenger ana kiburi gani ndani ya timu mpaka hataki kufanya usajili wa maana??
Hebu check Man City itakavyotisha next season na lazima watakuwa ndani ya the Big Four

Powered By Blogger