Wednesday 1 July 2009

Real waikabidhi Pauni Milioni 80 Man U!!
Fergie amsifia Ronaldo!!!
Cristiano Ronaldo leo rasmi amekuwa Mchezaji wa Real Madrid baada ya Klabu hiyo kuilipa Manchester United kitita chote cha Pauni Milioni 80.
Sir Alex Ferguson, ambae jana aliripoti ofisini baada ya kuwa likizo, ametamka: ‘Kila mtu anamtakia kila la kheri! Cristiano alikuwa Mchezaji bora kwa Manchester United! Miaka yake 6 hapa Old Trafford ilimfanya awe Mchezaji Bora Duniani! Mchango wake ulichangia mafanikio makubwa ya Klabu hii alipokuwepo na kipaji, uwezo wa kufurahisha Washabiki pamoja na utu wake umemfanya apendwe na Washabiki dunia nzima!’
Vidic atoboa: ‘Mke wangu haipendi Manchester, mie ni Man U damu!!’
Nemanja Vidic amepasua kuwa alipata ofa za kwenda kucheza Klabu za AC Milan, Real Madrid na Barcelona lakini amezikataa kwa sababu ya mapenzi yake kwa Manchester United ingawa Mke wake hapendi kuishi Jiji la Manchester.
Vidic, anaesifiwa kuwa ni mmoja wa Mabeki wa Kati wazuri duniani tangu ahamie Manchester United, amesema: ‘Mke wangu Ana hana furaha na mtindo wa maisha ya Manchester lakini siwezi kubadilisha mawazo kwa sababu nina furaha kuchezea Man U! Nilipata ofa kutoka AC Milan, Real Madrid na Barcelona lakini nimezikataa na nikawa mkweli nikaenda kumwambia Bosi wangu Sir Alex Ferguson!’ Vidic anaongeza: ‘Walitaka kulipa ada ya Pauni Milioni 30 kwa uhamisho wangu! Sir Alex Ferguson akaniongezea malupulupu na sasa, ingawa silipwi kama Rooney au Rio, nalipwa kama Berbatov au Carrick! Ntabaki Man U mpaka 2012!’

No comments:

Powered By Blogger