Friday 3 July 2009

Straika Veterani wa Liverpool Ian Rush akiri Owen atazaliwa upya Man U!!!
Ian Rush anaamini kabisa kwamba kwenda Michael Owen Manchester United kutamfanya azaliwe upya na kurudisha namba yake kwenye Kikosi cha Timu ya Taifa ya England ambako amechezea mechi moja tu tangu kuanza kwa utawala wa Mtaliana Fabio Capello kama Meneja wa England.
Kwa wengi usajili wa Michael Owen Manchester United umekuja kwa mshangao mkubwa hasa ukichukulia historia ya Michael Owen ya miaka ya hivi karibuni ya kuumia mara kwa mara lakini Supastaa wa zamani na Mfungaji Veterani wa Liverpool Ian Rush yuko taofauti.
Ian Rush amesema: ‘Owen ni Mfungaji mzuri sana bila ubishi! Kwa Sir Alex Ferguson kumchukua si kucheza tombola na nina uhakika atawafungia mabao mengi sana! Angalia Ferguson alimchukua Larsson na ikawa ni mafanikio makubwa sana na Owen itakuwa hivyo hivyo!’
Ian Rush ameongeza kwa kusema Manchester United itamsaidia Owen kuitwa tena kuchezea England na hata kwenda Fainali Kombe la Dunia mwakani huko Afrika Kusini hasa kwa sababu Man U ina Wachezaji wazuri watakaomchezesha vizuri Owen na kumfanya ang’are.
Tovuti ya Manchester United imevamiwa na Washabiki wa Manchester United wakimpongeza Sir Alex Ferguson kwa kumchukua Michael Owen na wengi wameomba siku Man U ikicheza na Liverpool basi wangependa Michael Owen ndie afunge goli la ushindi dhidi ya maadui hao wakubwa wa Man U na Klabu ya zamani ya Owen.

No comments:

Powered By Blogger