Thursday 2 July 2009

Benzema aenda Real Madrid!!!!
Karim Benzema, umri miaka 21, ametangazwa na Klabu yake ya Lyon ya Ufaransa kuwa atanunuliwa na Real Madrid kwa Pauni Milioni 30 na dau hilo linaweza kupanda hadi Milioni 35 kutegemea na mafanikio yake huko Real Madrid.
Karim Benzema ni Mrafansa alieanza kucheza Lyon tangu akiwa na miaka 9 kwenye Timu ya Watoto na alianza kucheza Kikosi cha kwanza cha Timu hiyo akiwa na miaka 17.
Msimu wa mwaka 2007/8 Benzema alifunga mabao 31 katika mechi 51 na kuwapa Ubingwa wa Ufaransa Lyon lakini msimu uliokwisha amefunga jumla ya mabao 23 tu katika mechi zote alizocheza na Lyon ikaukosa Ubingwa wa Ufaransa kwa mara ya kwanza katika muda wa miaka minane.
Ingawa ilivumishwa Karim Benzema atanunuliwa na Sir Alex Ferguson kwenda Manchester United lakini hilo halikuwezekana kwa sababu tu Real Madrid huwa wanamtumia Mfaransa Zinedine Zidane aliekuwa Mchezaji wa Real na ambae sasa wamemfanya Balozi wao ili kuwarubuni Wafaransa wenzake.
Mkono wa Zidane pia umewazuia Manchester United na Klabu nyingine yeyote kumchukua Franck Ribery kutoka Bayern Munich kwa sababu tu mpaka sasa Real Madrid wanaonyesha nia ya kumtaka Ribery.
Mpaka sasa Real Madrid imeshawanunua pia Cristiano Ronaldo, Kaka na Mlinzi Raul Albiol kwa kitita kikubwa sana cha Pauni Milioni 148.
Nani atafuata? Ribery? Alonso? Fabregas?
NANI ANAJUA?

No comments:

Powered By Blogger