Sunday 28 June 2009

Scolari awalaumu Drogba, Cech na Ballack!!!
Luiz Felipe Scolari amedai kuwa baadhi ya Wachezaji wa Chelsea walikuwa hawamheshimu yeye wala jinsi alivyokuwa akifundisha alipokuwa Meneja wa Chelsea kwa kipindi cha miezi minane.
Scolari, umri miaka 60, sasa ndie Kocha wa Klabu ya Uzbekistan iitwayo Bunyodkor, amewataja Didier Drogba kutoka Ivory Coast, Mjerumani Michael Ballack na Kipa kutoka Czech, Petr Cech, kuwa ndio waliokuwa na tabia hiyo isiyokubalika.
Scolari, alieanza kuifundisha Chelsea mwaka jana mwezi Julai na kutimuliwa Februari mwaka huu, amesema: ‘Kwa sasa Wamiliki wa Soka ni Wachezaji. Kocha, kwa Vilabu vingi Ulaya, hana ubavu wa kuwapinga!’
Scolari akaongeza: ‘Watu wanaofukuzwa siku zote ni Makocha! Wachezaji wakubwa wanajua hilo! Hilo ndio lilikuwa tatizo langu huko Chelsea!’
Scolari vilevile akaongelea juu ya uhamisho wa Ronaldo kwenda Real Madrid na kusema Kaka na Ronaldo watapatana na kuwa na uhusiano mzuri.
Scolari ni Mbrazil hivyo anamjua vizuri Kaka na alishawahi kuwa Kocha wa Ronaldo kwenye Timu ya Taifa ya Ureno.
Scolari ametamka: ‘Kaka ni mtu bora kiwanjani na nje! Ingawa amepata sifa kubwa na ni tajiri, Kaka siku zote anajituma uwanjani! Wataelewana ila tatizo ni Raul! Huyo ni veterani na ndio Bosi kwenye Vyumba vya Kubadilishia Jezi! Huenda kukatokea mfarakano kama hampendi mtu!’

No comments:

Powered By Blogger